Wafanyabiashara Soko la Miembeni Waazimia Kulinda Usafi
Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Wafanyabiashara wa Soko la Miembeni jijini Dodoma wameahidi kuendelea kuimarisha usafi wa mazingira katika maeneo yao ya biashara, wakieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kulinda afya na ustawi wa jamii. Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu wa Soko la Miembeni, Adelgot Mbwani alisema kuwa uongozi wa soko unaendelea kuwahamasisha wafanyabiashara kufanya usafi mara kwa mara na kuhakikisha kila mmoja anawajibika kutunza mazingira yanayomzunguka katika eneo lake la biashara. Aliongeza kuwa juhudi hizo pia zinaendana na msisitizo wa serikali wa kuhakikisha miji na maeneo ya biashara yanakuwa safi, hivyo wafanyabiashara wataendelea kushiriki kikamilifu katika kampeni za usafi. “Tumekuwa tukiwahamasisha wafanyabiashara wetu kufanya usafi mara kwa mara na kuwasisitizia kuwa usafi ni jukumu lao katika maeneo yao ya kazi, kama ambavyo Mheshimiwa Rais anavyosisitiza kuwa majiji yote yawe safi,” alisema Mbwani. Kwa upande wake, Katibu wa Soko la Wauza ...
Comments
Post a Comment