Polisi yaokoa fedha, yaongeza ujenzi wa jengo la ghorofa tatu mradi wa makazi Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Jeshi la Polisi Wilaya ya Dodoma limepongezwa kwa kufanikiwa kuokoa fedha katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa majengo ya makazi ya askari wa vyeo vya ‘rank and file’ hatua iliyowezesha kuongeza jengo moja la ghorofa tatu licha ya mradi awali kulenga kujenga majengo manane. Akizungumza wakati wa kukagua maendeleo ya mradi huo eneo la Kutuliza Ghasia Jiji la Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alikipongeza Kikosi Kazi cha Ujenzi cha Jeshi la Polisi kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa ufanisi na kuwezesha kuokoa fedha za umma. Alisema kuwa hatua hiyo ni mfano wa namna taasisi za serikali, hususan vyombo vya ulinzi na usalama, zinavyoweza kutanguliza uzalendo na matumizi bora ya fedha za umma katika kutekeleza miradi ya maendeleo. “Kwa hili tunawapongeza kwa dhati. ‘Mme-demonstrate’ kama vyombo vya ulinzi na usalama mkipewa majukumu haya ya nchi, mnatanguliza mbele uzalendo na kuokoa fedha za umma. Hili ni...