Elimu ya MEMKWA, Fursa ya Pili
Na. Muhamad Kulele, DODOMA
Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amesema kuwa
elimu ya MEMKWA imeendelea kuwa daraja muhimu kwa wale ambao hawakupata nafasi
ya kuendelea na elimu katika mfumo wa kawaida.
Mwakilishi huyo ambae ni Afisa Elimu wa Mkoa wa Dodoma, Kiduma Mageni alisema hayo alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma katika kilele cha Juma la Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi, kilichofanyika katika viwanja vya Nyerere Square, jijini Dodoma.
Alisema kuwa elimu ya MEMKWA imeendelea kuwa daraja
muhimu kwa wale ambao hawakupata nafasi ya kuendelea na elimu katika mfumo wa
kawaida. Alisema kuwa yeye binafsi ameshuhudia jitihada za MEMKWA katika
kuwapatia wananchi fursa ya kusoma, kuandika, kuhesabu na kujenga ujuzi wa
maendeleo.
Aidha, alisisitiza kuwa elimu haina umri, fursa ya
kujifunza haipaswi kufungwa na wakati.
Comments
Post a Comment