Timu ya Jiji la Dodoma yatakiwa kudumisha nidhamu mashindano ya SHIMISEMITA

Na. Mwandishi Wetu, DODOMA

Wachezaji wanaojiandaa kushiriki mashindano ya SHIMISEMITA watakiwa kuwa na malengo makubwa, nidhamu na ari ili kuweza kupata ushindi.



Hayo aliyasema Mwenyekiti wa SHIMISEMITA Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Gerald Ruzika wakati wa kikao chake na washiriki wa timu ya Jiji la Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutaho wa halmashauri jijini Dodoma.

Aliseama kuwa malengo yetu ni kupambania nafasi ya juu. “Mnakwenda kuiwakilisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Muwe na malengo ya ushindi na mkapambane kuurudisha ubingwa kama mlivyofanya mwaka jana. Fanyeni mazoezi kwa bidii, muwe na nidhamu na mshikamano ili mkaandike historia nyingine ya mafanikio,” alisema Dkt. Ruzika.

Aidha, aliwasisitiza washiriki kuongeza juhudi katika mazoezi na kuzingatia maelekezo ya makocha wao ili kuhakikisha wanakuwa katika kiwango bora kitakachowawezesha kufanya vizuri na kuipeperusha vema bendera ya Jiji la Dodoma.

Kwa upande wake, Nahodha wa Mpira wa Pete, Mwajuma Banyasa, alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na kila mshiriki ameonesha ari ya ushindani, jambo linalowapa imani ya kufanya vizuri kwenye mashindano hayo. “Tunafanya mazoezi kwa bidii na maandalizi yetu ni mazuri. Tuna imani kubwa ya kurudi na ushindi. Kwa wapinzani wetu nawaambia tu, tumejipanga vya kutosha na ushindi ni wa Jiji la Dodoma” alisema Banyasa.







Comments

Popular Posts

Jiji la Dodoma lashauriwa kulinda hadhi ya Makao Makuu ya Nchi