Vijana watakiwa kujiendeleza nje ya mfumo rasmi
Na. Lulu Luvanda, DODOMA Jamii imetakuwa kuwahamasisha vijana waliokosa elimu katika mfumo rasmi kujiunga na Mpango wa Elimu Changamani kwa Vijana walio nje ya shule nchini Tanzania (IPOSA) ili kupata fursa ya kujiendeleza kielimu nje ya mfumo rasmi. Akizungumza katika maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu wazima na nje ya mfumo rasmi yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere square, Afisa Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi wa Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, Annamaria Kidunda, alisema kuwa IPOSA inalenga kuwapa fursa vijana na wanafunzi ambao walishindwa kuendelea na mfumo rasmi wa elimu kupata nafasi nyingine ya kupata elimu nje ya mfumo rasmi. Kwa mujibu wa Kidunda, IPOSA ni darasa linalowahusisha wanafunzi waliokatisha masomo au kushindwa kuendelea na mfumo rasmi wa elimu, kwa kuwawezesha kupata elimu na mafunzo yatakayowasaidia kukabiliana na mahitaji ya maisha ya sasa. Alisema kuwa programu hiyo inalenga kuondoa pengo katika elimu kwa kuwapatia wa...
Comments
Post a Comment