Kanda Namba Moja yaadhimisha Miaka 62 ya Muungano kwa kufanya Usafi
Viongozi
wa Kanda Namba Moja, viongozi wa kata na mitaa pamoja na wafanyabiashara na
wananchi kwa ujumla, wameungana kushiriki zoezi la usafi katika Kata ya Uhuru
kwa kusafisha mitaro ya maji ya mvua iliyopo kando ya barabara. Zoezi hilo
limefanyika kwa lengo la kuimarisha usafi wa mazingira na kuhakikisha usalama
wa afya za wananchi. Aidha, zoezi hilo lilifanyika ikiwa sehemu ya maandalizi
ya kuelekea katika maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar, yenye kaulimbiu isemayo: "Miaka 62 ya Muungano: Amani na
Mshikikamano ni Msingi wa Maendeleo Endelevu".
Kupitia zoezi hilo, wananchi walikumbushwa umuhimu wa kudumisha usafi wa mazingira kila siku, bila kusubiri usafi wa jumamosi ya mwisho wa mwezi au wakati wa maadhimisho ili kujenga jamii yenye afya bora na maendeleo endelevu.
Comments
Post a Comment