Bucha 59 za uuzaji nyama Kanda Namba Sita zakaguliwa
Na. Mwandishi Wetu, MIYUJI
Timu ya wataalamu kutoka Kanda Namba Sita imefanya
operesheni maalum ya kukagua bucha za nyama na samaki, lengo likiwa ni
kudhibiti uuzaji wa nyama ambayo haijakaguliwa wala kupigwa muhuri na mamlaka
husika ili kulinda afya za walaji.
Akizungumza wakati wa kuhitimisha zoezi lililofanyika
takribani kwa siku tatu, Afisa Mifugo Kanda Namba Sita, Prisca Henry alisema
kuwa jumla ya bucha 59 zimekaguliwa ambapo ukaguzi uliofanyika ulihusisha
leseni, usafi wa bucha na vifaa vya kuhifadhia nyama na samaki na uvaaji wa
sare kwa wauzaji.
“Zoezi hili limetufanya kujua jumla ya idadi ya bucha
zilizopo kwenye kanda hii, pia imetupa fursa ya kutoa elimu kwa wafanyabiashara
mmoja mmoja kuhusu usafi na umuhimu wa kulipa leseni, ushuru wa huduma na
upimaji wa afya kwa wauzaji” alisema Henry.
Alisema kuwa zoezi hilo ni endelevu na kila mwezi
watafanya ukaguzi ili kutokomeza uuzaji haramu wa nyama na mazao yatokanayo na
mifugo na samaki.
MWISHO
Comments
Post a Comment