Diwani Kerenge atoa shukrani kwa wananchi kumchagua

Na. Mwandhishi wetu, MNADANI

Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge awashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumchagua na kuonesha imani katika uongozi wake, akisisitiza umuhimu wa kushirikiana ili kuboresha maisha ya wananchi wa Mtaa wa Mnadani.




Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Mnadani alisema kuwa moja ya majukumu yake makuu ni kusikiliza kero za wananchi, kuzitatua kwa haraka kadri inavyowezekana na kuhakikisha maendeleo yanashikamana na mahitaji halisi ya wananchi.

“Najivunia kuwa kiongozi wenu, lakini nawaomba tushirikiane kwa moyo mmoja, kila kero yenu ni muhimu kwangu, na tutaendelea kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha matatizo yanapatiwa ufumbuzi” alisema Kerenge.

Aidha, alisisitiza kuwa mikutano kama hiyo ni nafasi muhimu ya wananchi kutoa maoni, mapendekezo na kushirikiana na uongozi wa kata ili kuhakikisha huduma zinaboreshwa, zinapatikana kwa wakati na zinakidhi mahitaji ya wananchi wote.

Diwani Kerenge aliahidi kuendelea kufuatilia na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi, huku akisisitiza kuwa maendeleo ya kata ya Mnadani yanahitaji ushirikiano kati ya viongozi na wananchi.




Comments

Popular Posts

Gari la Darasa Tembezi latoa elimu Mitaa ya Jiji la Dodoma

Dodoma Jiji FC yatangaza benchi la ufundi msimu wa 2025/2026

Kata ya Chamwino kipaumbele Lishe shuleni