Mil. 838 zakopeshwa wanawake, vijana na wenye ulemavu Jiji la Dodoma
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
Halmashauri
ya Jiji la Dodoma imetoa mikopo ya shilingi 838,775,212 kwa vikundi 54 katika
kipindi cha Mwaka wa Fedha 2024/2025 hadi kufikia Oktoba 2025/2026 kwa lengo la
kuviongezea mtaji wa kutekeleza shughuli za kujikwamua kiuchumi.
Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Juni hadi Oktoba, 2025 katika mkutano wa kwanza wa halmashauri baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani.
Alisema
kuwa vikundi 17 vya wanawake vilikopeshwa shilingi 274,334,000, vikundi 26 vya
vijana vilikopeshwa shilingi 460,041,212 na watu wenye ulemavu vikundi 11
vilikopeshwa shilingi 104,400,000.
Akiongelea
uchangiaji wa michango ya asilimia 10, alisema kuwa mwaka 2024/2025 halmashauri
ilitenga shilingi 4,032,510,000, kwa mwezi Juni, 2024/2025, jumla ya shilingi
373,778,597.12 zimechangiwa katika mfuko. “Mwaka 2025/2026 halmashauri imetenga
bajeti ya asilimia 10 shilingi 4,421,659,500, shilingi 1,151,921,429.67
zimechangiwa hadi kufikia Oktoba, 2025” alisema Dkt. Sagamiko.
Wakati
huohuo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri aliipongeza Halmashauri
ya Jiji la Dodoma kwa kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya mfuko
wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Aidha, aliitaja halmashauri hiyo
kuwa ni kinara kwenye matumizi ya fedha hizo kwa walengwa.
MWISHO
Comments
Post a Comment