Jiji la Dodoma lakusanya 104% Mapato ya ndani 2024/2025

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma ilikusanya shilingi 65,042,215,034 sawa na asilimia 104 ya lengo la mwaka la mapato ya ndani kwa Mwaka wa Fedha 2024/ 2025.


Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Juni hadi Oktoba, 2025 katika mkutano wa kwanza wa halmashauri baada ya uchaguzi mkuu wa Rais, Watunge na Madiwani.

Alisema kuwa baada ya kuvunjwa kwa Baraza la Madiwani Mwaka 2025/2026 Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliendelea na jukumu la kukamilisha ukusanyaji wa mapato kwa kipindi cha mwaka 2024/2025. “Kwa Mwaka huo wa fedha, halmashauri ilikusudia kukusanya shilingi 143,164,202,949.46 na hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2025, ukusanyaji wa mapato ya ndani ulikuwa shilingi 65,042,215,034 sawa na asilimia 104 ya lengo la mwaka na kufanya ukusanyaji wa mapato yote ya halmashauri kuwa shilingi 152,269,204,654 sawa na asilimia 106” alisema Dkt. Sagamiko.

Alisema kuwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 halmashauri iliidhinishiwa kukusanya na kupokea jumla ya shilingi 164,579,966,999.99 ikiwa ni mapato yatokanayo na vyanzo vya ndani, ruzuku ya mishahara, ruzuku ya matumizi mengineyo na fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo. “Kwa kipindi cha Julai hadi Oktoba, 2025, jumla ya shilingi 22,193,124,132.17 zimekusanywa sawa na asilimia 30.96 ya lengo la makisio ya mwaka” alisema Dkt. Sagamiko.

Wakati huohuo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri  aliwataka madiwani kusimamia ukusanyaji wa mapato ya halmashauri. “Mstahiki Meya, nendeni mkasimamie halmashauri yetu iendelee kuwa mahili katika kukusanya mapato, mmepewa taarifa hapa kwamba asilimia 104 ya mapato imekusanywa na kuvuka lengo la mwaka ulioisha.

MWISHO 

Comments

Popular Posts

Watumishi wa Kanda Namba Tatu watembelea Zahanati ya Soweto

Gari la Darasa Tembezi latoa elimu Mitaa ya Jiji la Dodoma