Madiwani Jiji la Dodoma watakiwa kutoa tamko la rasilimali na madeni

                                             

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

SEKRETARIETI ya Maadili ya Viongozi wa Umma imewataka madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutoa tamko la rasilimali na madeni kwa mujibu wa sheria.


Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Msaidizi Kanda ya Kati, Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jasmin Bakari wakati akiwaongoza kutoa tamko la kimaandishi la ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

“Niwapongeze kwa kufanikiwa kuchaguliwa kuwa madiwani, ni mategemeo yetu mtatekeleza majukumu yenu kwa viwango vya juu vya maadili, na mviishi viapo vyenu. Niwakumbushe madiwani na viongozi wote waliopo hapa kutoa tamko la rasilimali na madeni, tunawakumbusha kuingia kwenye mfumo kwa wale wapya kuna sehemu ya kujisajili. Kwa wale waliokuwa baraza lililopita wataingia kwa akaunti zao za awali” alisema Bakari. 

Nae, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, Charles Mamba aliiomba kamati ya maadili ianze kazi mapema ili kuondoa makundi na chuki. “Katibu, nashauri kwamba kamati ya madili ianze kufanya kazi mapema iwezekanavyo. Tuna matarajio na uwepo wenu katika baraza hili. Saidianeni ili kuvushana katika utendaji kazi” alisema Mamba.

Alimalizia kusema kuwa, madiwani watumie weledi katika kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili wananchi wanufaike moja kwa moja.

Katika hatua nyingine, Diwani wa Kata ya Mpunguzi, Isaya Chilongani alipongeza uundwaji wa baraza na kuahidi kutoa ushirikiano katika utendaji kazi. “Namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa siku ya leo, kuanza rasmi kwa baraza hili ni ishara kuwa tuna nafasi kubwa sana ya kuwatumikia wananchi. Nipo tayari kutoa ushirikiano kwa madiwani wenzangu na wananchi ili kufanikisha lile lengo la kuleta maendeleo katika kata zetu” alipongeza Chilongani.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Watumishi wa Kanda Namba Tatu watembelea Zahanati ya Soweto

Gari la Darasa Tembezi latoa elimu Mitaa ya Jiji la Dodoma