Posts

Maendeleo ya Miradi Kata ya Makole

Na. Jackline Patrick, DODOMA Maendeleo ya kata ya makole yanatokana na serikali kupeleka fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo inayoboresha maisha ya wananchi. Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa kata ya Makole, Omary Haji alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari nje ya ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya jiji la Dodoma kuhusu maendeleo ya kata ya makole. "Maendeleo ya Kata ya Makole yanatokana na miradi ya maendeleo ambayo imeanzishwa. Kata ina miradi mikubwa mingi kuna ujenzi wa madarasa kiwango cha ghorofa, uliogharimu takribani shilingi milioni 500. Tunamiradi tofauti tofauti ili kuweza kukamilisha miradi hiyo lazima kuwe na jitihada" alisema Haji. Vilevile, Kata ya Makole "inaujenzi katika eneo la D center na Ofisi ya wamachinga Jijini Dodoma. Katika maendeleo haya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo pia amechochea miradi kusonga mbele, haisuisui, miradi haina viporo na kukamilika kwa wakati" alisisitiza Haji. ...

Dodoma Jiji FC yaja kivingine

Image
Na. Fadiga James, DODOMA Timu ya Mpira wa Miguu ya Dodoma Jiji ambayo imekuwa ikishiriki ligi kuu nchini imeweka mikakati mizito kuelekea msimu mpya wa ligi kuu Tanzania Bara (NBC premier league) unaotarajia kuanza hivi karibuni.   Mikakati hiyo ilitajwa na Diwani wa Kata ya Makole, Omary Haji alipokuwa akiongea na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuhusiana na maandalizi ya Dodoma Jiji FC kuelekea kuanza kwa ligi kuu. Diwanni Haji alisema kuwa timu hiyo imejiwekea mikakati kwenye msimu mpya wa mashindano unaotarajia kuanza mwisho mwa mwezi Agosti, 2024 kuwa ni kushinda mechi zote. ‘Mimi kama mdau wa Dodoma Jiji FC kwanza najivunia na kujisikia fahari kuwa na timu inayoshiriki ligi kuu. Kwahiyo, cha kwanza wananchi wetu wa Dodoma watafurahia kuangalia mechi kwa timu zinazoshiriki ikiwemo Simba, Yanga na Azam na timu nyingine kwasababu lazima zije kucheza hapa. Sisi kama Dodoma Jiji FC tulikaa wakati tunavunja kambi na Mkurugenz...

Baraza la Madiwani Dodoma lampongeza Rais fedha za miradi

Image
Na. John Masanja, KATA YA VIWANDANI   Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lampongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuhakikisha serikali inapeleka fedha za kutosha katika maendeleo na kutekeleza ujenzi wa miradi mbalimbali nchini hususani ndani ya Jiji la Dodoma.   Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe Hayo yalisemwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kuwasilisha taarifa za utekelezaji kutoka kwenye kata, uliofanyinya katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   “Hakuna ubishi wowote kuhusu jinsi serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ilivyopoleka pesa kwa ajili ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya nchi, hili halina ubishi” alisema Prof. Mwamfupe.   Aidha, Pro. Mwamfupe aliwata wajumbe wa mkutano huo kuendelea kutoa u...

Madiwani Jiji la Dodoma washauriwa kushirikiana na wadau wa maendeleo

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo amewashauri madiwani kujenga uhusiano mzuri na wadau wa maendeleo waliopo katika kata ili wasaidie kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Mkurugenzi wa Jiji, John Kayombo akifafanua jambo Kayombo alitoa kauli hiyo katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kuwasilisha taarifa za utekelezaji kutoka kwenye kata uliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Kayombo alisema “wadau wa maendeleo kwenye kata wapo wengi tuwatumie ili kuunga mkono utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata”. MWISHO

Wanafunzi wa ‘field’ wapelekwe kwenye kata

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MSTAHIKI Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe amewataka wanafunzi wanaofanya mafunzo kwa vitendo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwenda kwenye kata kufanya kazi za jamii ili kupata uzoefu tofauti. Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe Kauli hiyo aliitoa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kuwasilisha taarifa za utekelezaji kutoka kwenye kata uliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Prof. Mwamfupe alisema “idadi ya wanafunzi wa ‘field’ ni kubwa, waende kwenye kata kufanya kazi za jamii. Wapo waandishi wa habari hapa, habari hazipo kwa Mstahiki Meya na Mkurugenzi pekee, waende kwenye kata. Hii itawanufaisha wao kwa kupata uzoefu na kutakuwa na mafuriko ya habari zinazohusu kata na maendeleo ya wananchi”. Kwa upande wake Flora Nadoo alisema kuwa kauli ya Mshahiki Meya ni nzuri kwa sababu wanavyoenda kwenye kata wanajifunza vitu vingi na kujua changamoto zinazowakabili wananchi moja ...

Madiwani Jiji la Dodoma washauriwa kutafsiri miradi ya maendeleo kwa wananchi

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kutafsiri kwa vitendo maana ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika kubadilisha maisha ya watu na kuyafanya kuwa bora kuliko jana. Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani, Prof. Davis Mwamfupe akielezea miradi maana ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya sita. Kulia kwake ni mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma ambae ni Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA, Joseph Fungo  Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe wakati akifungua mkutano wa Baraza la Madiwani wa kuwasilisha taarifa za utekelezaji kutoka kwenye kata kwa kipindi cha robo ya nne (Aprili-Juni, 2024) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Prof. Mwamfupe ambae pia ni Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema “hakuna ubishi wowote jinsi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu H...

Rais, Dkt. Samia: SGR siyo ndoto tena

Image
Na. Janeth Gerald, KIKUYU KUSINI Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua treni ya mwendokasi (Standard Gauge Railway) na kuandika historia baada ya miaka 114 ya Tanzania kujenga reli ndefu na kusema kuwa mradi wa SGR siyo ndoto tena, bali ni uhalisia. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa miundombinu na safari za treni kati ya Dar es salaam na Dodoma kupitia Morogoro alisema kuwa aliupokea mradi huo kutoka kwa watangulizi wake na kuufikisha hapo. Alisema kuwa katika miaka mitatu ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita, wamekamilisha ujenzi wa vipande viwili vya Dar es salaam hadi Morogoro na Morogoro hadi Dodoma. "Kwa sasa kazi inaendelea katika vipande vya Makutupora hadi Tabora kilometa 368, Tabora hadi Isaka kilometa 341, na Isaka hadi Mwanza kilometa 341. Pia serikali inajenga Tabora hadi Kigoma, kipande chenye urefu wa kilometa 565, ambayo itajumuisha kuingia katika nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Nchi zilizoendelea hazikutaka kuona Tanzania ina...

Rais Samia asisitiza kuendelezwa kwa ubora wa reli ya SGR

Image
Na. Fadiga James, KIKUYU KUSINI Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amelitaka Shirika la Reli nchini (TRC) kuhakikisha ujenzi wa reli ya SGR unaendelea kufanyika kwa ubora wa hali ya juu. Agizo hilo alilitoa wakati wa uzinduzi wa stesheni ya SGR Dodoma iliyopo Kata ya Kikuyu Kusini jijini Dodoma. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alisema kuwa TRC na menejimenti yake kusimamia ujenzi wa reli ya SGR kwa ubora wa hali ya juu. Reli ikijengwa vizuri itaweza kudumu kudumu na kunufaisha nchi kwa muda mrefu, aliongeza. "Bodi ya wakurugenzi na menejimenti ya TRC, hakikisheni vipande vya reli hii inayoendelea kujengwa ya SGR, vinakamilika kwa wakati na ubora uliokubariwa" alisema. Vilevile, aliiagiza TRC kuhakikisha huduma zinazotolewa ndani na nje ya treni zinakuwa za ubora ili kuvutia zaidi watalii wa ndani na nje ya nchi na kuhakikisha usalama wa abiria na mali zao ndani ya treni hiyo. MWISHO

RC aishukuru Serikali kupeleka Nanenane kitaifa Dodoma

Image
Na. Fadiga James, NANENANE Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameishukuru serikali kwa kuamua maonesho ya Nanenane kitaifa kufanyikia Dodoma na kusema ni fursa kwa wananchi wa mkoa huo kunufaika kiuchumi. Senyamule alitoa shukrani hizo wakati akitoa salamu za Mkoa wa Dodoma kwenye ufunguzi wa maonesho ya Nanenane kitaifa yaliyofanyika Kanda ya Kati uliofanywa na Waziri Mkuu wa Tanzania katika viwanja vya Nanenane, Nzuguni jijini Dodoma. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanikisha sherehe za Nanenane kufanyika jijini Dodoma na kusema kuwa ni mahali sahihi kwasababu wakulima na wafugani ni wengi na yatasaidia wananchi kukua kiuchumi. “Kipekee nishukuru sana kwa dhati kuwa mwaka huu 2024 maonesho ya Nanenane yanafanyika Kanda ya Kati kitaifa katika Mkoa wa Dodoma. Tunashukuru sana kwasababu ni historia ya muda mrefu kidogo, tulishaanza kusahau kuandaa hata haya maonesho ya kimataifa, lakini tutoe shukrani nyingi kwa mheshi...

Wafanyabiashara wanufaika na ufunguzi wa Nanenane na uzinduzi wa SGR

Image
Na. Rahma Abdallah, NANENANE NA KIKUYU KUISNI Wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamenufaika kutokana na ufunguzi wa maonesho ya siku ya Nanenane yaliyofanyika katika viwanja vya Nanenane Nzuguni jijini Dodoma pamoja na ufunguzi wa treni ya kisasa ya mwendo kasi inayotumia umeme (SGR), ufunguzi huo uliofanyika Kata ya Kikuyu Kusini jijini Dodoma.   Hayo yamezungumzwa na wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma mapema jana katika ufunguzi wa maonesho ya Nanenane pamoja ufunguzi wa Treni ya kisasa inayotumia umeme (SGR). “Nashukuru Mungu mimi nikiwa kama mfanyabiashara wa chakula nimenufaika sana kwa sababu watu ni mengi sana hatuna budi kumenya viazi vingi ili wateja wetu wanapokuja kukuta kila kitu kiko vizuri pia kupitia ufunguzi huu sisi kama wafanyabiashara tumepata fursa kwasababu kabla ya uzinduzi huu biashara haikuwa nzuri kabisa kwa sababu ya ukosefu wa watu (wateja) lakini kwa kupitia uzinduzi huu tumechangamkia na kufanya biashara’’ alisema ...