RC aishukuru Serikali kupeleka Nanenane kitaifa Dodoma

Na. Fadiga James, NANENANE

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameishukuru serikali kwa kuamua maonesho ya Nanenane kitaifa kufanyikia Dodoma na kusema ni fursa kwa wananchi wa mkoa huo kunufaika kiuchumi.



Senyamule alitoa shukrani hizo wakati akitoa salamu za Mkoa wa Dodoma kwenye ufunguzi wa maonesho ya Nanenane kitaifa yaliyofanyika Kanda ya Kati uliofanywa na Waziri Mkuu wa Tanzania katika viwanja vya Nanenane, Nzuguni jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanikisha sherehe za Nanenane kufanyika jijini Dodoma na kusema kuwa ni mahali sahihi kwasababu wakulima na wafugani ni wengi na yatasaidia wananchi kukua kiuchumi.

“Kipekee nishukuru sana kwa dhati kuwa mwaka huu 2024 maonesho ya Nanenane yanafanyika Kanda ya Kati kitaifa katika Mkoa wa Dodoma. Tunashukuru sana kwasababu ni historia ya muda mrefu kidogo, tulishaanza kusahau kuandaa hata haya maonesho ya kimataifa, lakini tutoe shukrani nyingi kwa mheshimiwa Rais, lakini tutoe shukrani nyingi kwa Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa uamuzi huu” alisema Senyamule.

Akitumia ufunguzi huo kuwataka wakazi wa Dodoma kuchangamkoa fursa ya maonesho hayo kufanyikia Dodoma kukua kiuchumi. Alisema kuwa ni fursa kwa makundi yote kuchangamka kujifunza teknolojia mpya za kilimo na ufugaji na kunufaika na wingi wa watu kufanya biashara mbalimbali na kukua kiuchumi.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma