Maendeleo ya Miradi Kata ya Makole


Na. Jackline Patrick, DODOMA

Maendeleo ya kata ya makole yanatokana na serikali kupeleka fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo inayoboresha maisha ya wananchi.



Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa kata ya Makole, Omary Haji alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari nje ya ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya jiji la Dodoma kuhusu maendeleo ya kata ya makole.

"Maendeleo ya Kata ya Makole yanatokana na miradi ya maendeleo ambayo imeanzishwa. Kata ina miradi mikubwa mingi kuna ujenzi wa madarasa kiwango cha ghorofa, uliogharimu takribani shilingi milioni 500. Tunamiradi tofauti tofauti ili kuweza kukamilisha miradi hiyo lazima kuwe na jitihada" alisema Haji.

Vilevile, Kata ya Makole "inaujenzi katika eneo la D center na Ofisi ya wamachinga Jijini Dodoma. Katika maendeleo haya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo pia amechochea miradi kusonga mbele, haisuisui, miradi haina viporo na kukamilika kwa wakati" alisisitiza Haji.

Kata ya Makole zilitolewa fidia kwa wananchi wapatao sita katika eneo la ‘D center’ Makole ambao wameshalipwa zaidi ya shilingi milioni sita pamoja na miradi mingi ya serikali ya kimikakati.

Diwani huyo aliongeza kwa kusema kuwa alianzisha Diwan Cup katika Kata ya Makole kwa sababu kata hiyo ipo vizuri kimichezo.

Habari hii mehaririwa na Emmanuel Lucas

MWISHO

Comments

Popular Posts

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala

Kata ya Ipala ipo mstari wa mbele katika Michezo