Baraza la Madiwani Dodoma lampongeza Rais fedha za miradi

Na. John Masanja, KATA YA VIWANDANI

 

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lampongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuhakikisha serikali inapeleka fedha za kutosha katika maendeleo na kutekeleza ujenzi wa miradi mbalimbali nchini hususani ndani ya Jiji la Dodoma.

 

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe


Hayo yalisemwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kuwasilisha taarifa za utekelezaji kutoka kwenye kata, uliofanyinya katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

 

“Hakuna ubishi wowote kuhusu jinsi serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ilivyopoleka pesa kwa ajili ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya nchi, hili halina ubishi” alisema Prof. Mwamfupe.

 

Aidha, Pro. Mwamfupe aliwata wajumbe wa mkutano huo kuendelea kutoa ujumbe na elimu kwa wananchi kuhusu jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita katika kutekeleza ujenzi wa miradi hiyo pamoja na uboreshwaji wa huduma, zinavyoleta manufaa kwa jamii na kuzitazama fursa mbalimbali zilizopo kwenye ujio wa miradi hiyo.

 

“Twendeni zaidi kwa wananchi wetu wa kawaida na kuwaeleza, wazitumieje fursa hizo zilizopo kwenye ujio wa miradi mbalimbali kama huu wa Treni ya Mwendokasi (SGR)” aliongeza Prof. Mwamfupe.

 

Akizungumza mara baada ya uwasilishwaji wa taarifa hizo, Daudi Mkhandi, Diwani wa Kata ya Nkuhungu, aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa miradi na kusema kuwa imesaidia kupunguza kadhia mbalimbali kwa wananchi huku akishauri kumaliziwa kwa miradi viporo katika mwaka mpya wa fedha 2024/25.

 

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kilimani, Neema Mwaluko alisema kwa mara ya kwanza ndani ya mwaka wa fedha 2023/24, Kata ya Kilimani imefanikiwa kujegewa Shule mpya ya Msingi ya kwanza ya Chinyoya na kusema kuwa kupitia uwepo wa shule hiyo utakwenda kupunguza changamoto ya umbali kwa wananfunzi waliokuwa wakienda kusoma katika maeneo ya mbali na wanapoishi.

 

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala

Shilingi Bilioni 7 zatekeleza miradi ya maendeleo Kata ya Miyuji