Rais, Dkt. Samia: SGR siyo ndoto tena

Na. Janeth Gerald, KIKUYU KUSINI

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua treni ya mwendokasi (Standard Gauge Railway) na kuandika historia baada ya miaka 114 ya Tanzania kujenga reli ndefu na kusema kuwa mradi wa SGR siyo ndoto tena, bali ni uhalisia.




Akizungumza wakati wa uzinduzi wa miundombinu na safari za treni kati ya Dar es salaam na Dodoma kupitia Morogoro alisema kuwa aliupokea mradi huo kutoka kwa watangulizi wake na kuufikisha hapo.

Alisema kuwa katika miaka mitatu ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita, wamekamilisha ujenzi wa vipande viwili vya Dar es salaam hadi Morogoro na Morogoro hadi Dodoma.

"Kwa sasa kazi inaendelea katika vipande vya Makutupora hadi Tabora kilometa 368, Tabora hadi Isaka kilometa 341, na Isaka hadi Mwanza kilometa 341. Pia serikali inajenga Tabora hadi Kigoma, kipande chenye urefu wa kilometa 565, ambayo itajumuisha kuingia katika nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Nchi zilizoendelea hazikutaka kuona Tanzania inakamilisha mradi huu wa SGR kwasababu zinafahamu kuwa mradi huu ukikamilika Tanzania inafuta umasikini. Pia kuna mzigo mkubwa kati ya nchi ya DRC na nchi nyingine jirani ambao utasaidia Bandari ya Dar es salaam kuwa na mzigo wa kutosha na kutengeneza faida kubwa" alisema Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, alilitaka Shirika la Reli nchini kuendesha treni hiyo kibiashara na kutotegemea ruzuku ya serikali bali kutoa gawio la mwaka kwa serikali baada ya kutengeneza faida.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma