Madiwani Jiji la Dodoma washauriwa kushirikiana na wadau wa maendeleo

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo amewashauri madiwani kujenga uhusiano mzuri na wadau wa maendeleo waliopo katika kata ili wasaidie kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Mkurugenzi wa Jiji, John Kayombo akifafanua jambo


Kayombo alitoa kauli hiyo katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kuwasilisha taarifa za utekelezaji kutoka kwenye kata uliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri.

Kayombo alisema “wadau wa maendeleo kwenye kata wapo wengi tuwatumie ili kuunga mkono utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata”.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

Shilingi Bilioni 7 zatekeleza miradi ya maendeleo Kata ya Miyuji

Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota