Dodoma Jiji FC yaja kivingine


Na. Fadiga James, DODOMA

Timu ya Mpira wa Miguu ya Dodoma Jiji ambayo imekuwa ikishiriki ligi kuu nchini imeweka mikakati mizito kuelekea msimu mpya wa ligi kuu Tanzania Bara (NBC premier league) unaotarajia kuanza hivi karibuni.

 




Mikakati hiyo ilitajwa na Diwani wa Kata ya Makole, Omary Haji alipokuwa akiongea na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuhusiana na maandalizi ya Dodoma Jiji FC kuelekea kuanza kwa ligi kuu.

Diwanni Haji alisema kuwa timu hiyo imejiwekea mikakati kwenye msimu mpya wa mashindano unaotarajia kuanza mwisho mwa mwezi Agosti, 2024 kuwa ni kushinda mechi zote.

‘Mimi kama mdau wa Dodoma Jiji FC kwanza najivunia na kujisikia fahari kuwa na timu inayoshiriki ligi kuu. Kwahiyo, cha kwanza wananchi wetu wa Dodoma watafurahia kuangalia mechi kwa timu zinazoshiriki ikiwemo Simba, Yanga na Azam na timu nyingine kwasababu lazima zije kucheza hapa. Sisi kama Dodoma Jiji FC tulikaa wakati tunavunja kambi na Mkurugenzi wa Jiji, mkurugenzi ana mikakati mingi sana mizuri na nina imani kabisa Dodoma Jiji FC itafanya vizuri msimu huu kwasababu tuna malengo madhubuti sana ili kuhakikisha Dodoma Jiji FC inafanya vizuri. Mechi zote za Dodoma za nyumbani inatakiwa tushinde ili tujiweke katika nafasi nzuri pamoja na mechi za ugenini’’ alisema Haji.

Pia licha ya mikakati na mpango mzuri kuelekea msimu mpya wa mashindano ambao ni kushinda mechi zake za nyumbani lakini Dodoma Jiji FC imeonekana kuwa na matokea mazuri kipindi hiki cha maandalizi ambapo timu iliweka kambi jijini Arusha. Kati michezo minne ya mwisho Timu ya Dodoma Jiji FC ilifanikiwa kuibuka na ushindi katika michezo yote huku ikitoshana nguvu katika mchezo mmoja na Fountain Gate FC.

Timu ya Dodoma Jiji FC imekuwa na muendelezo mzuri katika ligi kuu ya NBC ikiwa ni zaidi ya misimu mitatu sasa ikisalia katika ligi hiyo na kuendelea kutoa ushindani mzuri hususani kwa timu ambazo madaraja yao yanalingana.

Habari hii imehaririwa na Emmanuel Lucas

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma