Rais Samia asisitiza kuendelezwa kwa ubora wa reli ya SGR

Na. Fadiga James, KIKUYU KUSINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amelitaka Shirika la Reli nchini (TRC) kuhakikisha ujenzi wa reli ya SGR unaendelea kufanyika kwa ubora wa hali ya juu.



Agizo hilo alilitoa wakati wa uzinduzi wa stesheni ya SGR Dodoma iliyopo Kata ya Kikuyu Kusini jijini Dodoma.

Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alisema kuwa TRC na menejimenti yake kusimamia ujenzi wa reli ya SGR kwa ubora wa hali ya juu. Reli ikijengwa vizuri itaweza kudumu kudumu na kunufaisha nchi kwa muda mrefu, aliongeza.

"Bodi ya wakurugenzi na menejimenti ya TRC, hakikisheni vipande vya reli hii inayoendelea kujengwa ya SGR, vinakamilika kwa wakati na ubora uliokubariwa" alisema.

Vilevile, aliiagiza TRC kuhakikisha huduma zinazotolewa ndani na nje ya treni zinakuwa za ubora ili kuvutia zaidi watalii wa ndani na nje ya nchi na kuhakikisha usalama wa abiria na mali zao ndani ya treni hiyo.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma