Timu ya Watumishi Jiji la Dodoma inayoshiriki SHIMISEMITA yatakiwa kurejea na ushindi
Na. Lulu Luvanda, DODOMA Timu ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma itakayoshiriki Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) wametakiwa kulitangaza vema jiji hilo katika michezo kwa kuzingatia nidhamu na misingi ya utumishi wa umma na kurejea na ushindi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko wakati wa tukio la kuwaaga wanamichezo hao watakaoshiriki michezo ya SHIMISEMITA jijini Mbeya. Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wachezaji hao iliyofanyika katika ukumbi wa halmashauri jijini Dodoma, alisema kuwa mashindano hayo ni fursa ya kulitangaza Jiji la Dodoma kupitia michezo, huku akiwataka wachezaji kuzingatia nidhamu, maadili na misingi ya utumishi wa umma. Alitumia hafla hiyo kumpongeza Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa, Neema Kilongola kwa mchango wake katika kuimarisha michezo ndani ya halmashauri hiyo, akisisitiza kuwa mafanikio ya ...
Comments
Post a Comment