Posts

JIJI LA DODOMA KUPELEKA MIL 50 ZAHANATI YA KIKUYU

Image
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KASKAZINI SERIKALI kupeleka shilingi milioni 50 kukamilisha jengo la wodi ya wazazi katika Zahanati ya Kikuyu iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa lengo la kuwafikishia huduma za afya wananchi. Mbunge Anthony Mavunde Kauli hiyo ilitolewa Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini, Anthony Mavunde alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi wa Kata ya Kikuyu Kaskazini waliojitokeza kushiriki zoezi la usafi wa mazingira na upandaji miti kuzunguka Zahanati ya Kikuyu. Mavunde alisema “Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma jengo unaloliona kushoto kwako ni jitihada zangu mimi na diwani wa hapa. Habari njema ni kwamba kabla ya Jumatano wiki ijayo tunaingiza shilingi milioni 50 ambazo zitakwenda kukamilisha jengo hilo. Na nategemea mwezi Oktoba mwaka huu kina mama wataanza kuhudumiwa katika wodi ya wazazi”. Akiongelea historia ya jengo hilo, alisema kuwa mwaka 2020 aliwaahidi wananchi wa kata hiyo kujengewa wodi ya wazazi. “Nilikuja hapa nikiwa na Diwani Mwansasu nikakut...

DC DODOMA APONGEZA ZAHANATI YA KIKUYU KUBORESHA MANDHARI

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri ameipongeza Zahanati ya Kikuyu kwa kuboresha mandhari na kuyafanya ya kuvutia na kupanda miti kwa lengo la kuwa na hewa safi. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shemimweri akiongea na mamia ya wananchi wa Kata ya Kikuyu Kaskazini Pongezi hizo alizitoa alipoongoza zoaezi la usafi wa mazingira na kupanda miti katika zahanati hiyo iliyopo katika Kata ya Kikuyu Kaskazini jijini Dodoma. Shekimweri alisema “niungane na Mheshimiwa Mbunge kuwapongeza kwa dhati Zahanati ya Kikuyu ikiongozwa na Mganga Mfawidhi kwa wazo la kuboresha mandhari ya zahanati yao. Ni dhamira yetu tutafute ‘model’ ya uangalizi wa mazingira katika maeneo yetu ya kutolea huduma ya afya. Mbunge amening’ata sikio kuwa atabadilisha paa siyo kwa kupaka rangi bali yeye ataleta mabati mapya”. Aidha, alitoa rai kwa vituo vingine vya afya kuboresha mandhari yake. “Rai kwa vituo vingine vya afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuboresha mandhari. Mganga...

WANANCHI CHAMWINO WAJITOKEZA USAFI WA MAZINGIRA

Image
Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO KATA ya Chamwino iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma yatekeleza zoezi la usafi wa kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kwa wananchi kijitokeza kwa wingi na kufanya usafi katika maeneo ya jumuiya. Zoezi la usafi likiendelea Afisa Mtendaji Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alisema kuwa zoezi la usafi wa pamoja wa kila siku ya Jumamosi ya mwisho wa mwezi lilifanyika katika mitaa minne ya kata hiyo. “Nikuhakikishie kuwa usafi wa Jumamosi ya mwisho wa mwezi umefanyika katika mitaa yote minne ya Kata ya Chamwino. Mtaa wa Nduka, Mailimbili, Sokoine na Mwaja” alisema Nkelege. Akiongelea maeneo yaliyofanyiwa usafi wa pamoja, aliyataja kuwa ni makorongo, kusafisha mitaro na maeneo ya biashara. “Mtaa wa Mwaja na Nduka iliungana na kufanya usafi wa pamoja katika korongo. Usafi huo ulihusisha kuondoa mifuko ya plastiki, kufyeka vichaka na nyasi zilizoota ndani ya korongo. Mtaa wa Mailimbili usafi wa pamoja ulifanyika katika mtaro wa barabara ya kwenda Arusha. Us...

DC SHEKIMWERI ASHAURI UTUNZAJI MAZINGIRA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KASKAZINI -DODOMA WAKAZI wa Wilaya ya Dodoma wametakiwa kutunza na kulinda Mazingira ili kujihakikishia uhai wa maisha ya wanadamu na viumbe hai. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri akipanda mti katika Zahanati ya Kikuyu Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipoongoza zoezi la usafi wa Mazingira na upandaji miti kuzunguka Zahanati ya Kikuyu iliyopo Kata ya Kikuyu Kaskazini jijini hapa. Shekimweri alisema kuwa uhai wa wanadamu upo kwenye mazingira safi yenye miti mizuri. “Nisisitize mambo machache kwenye zoezi la kupanda miti. Katika uumbaji Mwenyezi Mungu ametuumba kwa kutegemeane na mazingira hakuna namna maisha yetu yatakuwepo pasina uwepo wa miti kwenye mazingira yanayotuzunguka. Sisi tunatoa hewa inaitwa ‘carbon dioxide’ ambayo kwa uumbaji wa Mungu hiyo ndiyo hewa safi kwa miti. Na yenyewe inatoa hewa chafu ambayo inaitwa ‘oxygen’ ambayo kwa maisha ya wanadamu ndiyo hewa safi. Kwa hiyo tunabadilishana hewa chafu ...

MBUNGE MAVUNDE ASHIRIKI ZOEZI LA USAFI NA UPANDAJI MITI JIJI LA DODOMA TAREHE 29 JULAI, 2023

Image
 

DC SHEKIMWERI ASHIRIKI ZOEZI LA USAFI NA UPANDAJI MITI JIJI LA DODOMA TAREHE 29 JULAI, 2023

Image
 

AFISA MTENDAJI KATA YA CHAMWINO APEWA CHETI UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE JIJI LA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA AFISA Mtendaji wa Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege amepongezwa na kupatiwa cheti kwa kufanya vizuri katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe katika jijini Dodoma. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri akimkabidhi cheti kutambua kazi nzuri ya utekelezaji Mkataba wa Lishe Afisa Mtendaji Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Lishe Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipoongoza Kikao cha Tathmini ya Mkataba wa Lishe kwa robo ya nne kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Shekimweri ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma alisema kuwa suala la lishe ni muhimu kwa wilaya yake na maafisa watendaji wa kata wana wajibu wa kusimamia lishe katika maeneo yao. “Ndugu zangu, napenda kuwaambia tunatakiwa kuwa na tafsiri pana na dhamira ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusiana na suala la lishe. Tuhakikishe watoto wanapata chakula shuleni. Wale wote amb...

JIJI LA DODOMA KUPELEKA TIMU YA MAAFISA MAZINGIRA NA AFYA KUKAGUA USAFI KATA YA IPAGALA

Image
Na. Dennis Gondwe, IPAGALA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma kupeleka timu ya maafisa mazingira na afya kufanya ukaguzi katika maeneo ya Mtaa wa Ipagala kukagua hali ya usafi wa mazingira kutokana na changamoto wa baadhi ya wakazi wa maeneo hayo kutojitokeza kufanya usafi wa mazingira. Mkuu wa Kitengo cha Usafi na uthibiti taka ngumu Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro akiongea na mamia ya wakazi wa Ipagala Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na uthibiti wa taka ngumu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alipokuwa akiongea na mamia ya wakazi wa Kata ya Ipagala waliojitokeza katika usafi wa pamoja kwenye korongo la kitaa cheusi. Kimaro alisema “kwa sababu eneo hili lina changamoto ya wananchi kutojitokeza kufanya usafi katika maeneo yao. Wananchi wanalalamika kuwa watu wanaokaa kwenye nyumba zenye mageti hawajitokezi kufanya usafi na kuwaanchia wanaoishi katika nyumba zisizo na mageti kufanya usafi. Nimetoa maelekezo kwamba wiki ijayo kuanzia siku ya Jumatatu timu ya...

CANADA YATOA BILIONI 240 KWENYE MFUKO WA AFYA WA PAMOJA

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Serikali ya C anada imetoa kiasi cha s hilingi Bilioni 240 kwenye Mfuko wa Afya w a pamoja (Health Basket Fund) ili kusaidia s ekta ya Afya nchini. Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu Waziri wa Afya , Ummy Mwalimu a libainisha hayo Julai 20, wakati wa mkutano wa utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Afya wa p amoja (Health Busket Fund) na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada j ijini Dodoma. “Tunaishuku sana Serikali ya C anada kupitia Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa C anada , Mhe shimiwa Harjit Sajjan i kwa kusaidia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kiasi cha shilingi Bilioni 240 kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya”, a lishukuru Waziri Ummy . Aidha, alieleza kuwa kati ya kiasi hicho shilingi Bilioni 140 zinaingia serikalini kwa ajili ya kuchangia M fuko wa A fya wa Pamoja . Serikali i li shapokea kiasi cha shilingi Bilioni 94 ambazo zimeelekezwa kwenye akaunti za ngazi ya msingi ambazo ni zahanati na vituo vya afya nchin...

HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA YAPATA HATI SAFI YA UKAGUZI WA HESABU