DC DODOMA APONGEZA ZAHANATI YA KIKUYU KUBORESHA MANDHARI

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri ameipongeza Zahanati ya Kikuyu kwa kuboresha mandhari na kuyafanya ya kuvutia na kupanda miti kwa lengo la kuwa na hewa safi.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shemimweri akiongea na mamia ya wananchi wa Kata ya Kikuyu Kaskazini


Pongezi hizo alizitoa alipoongoza zoaezi la usafi wa mazingira na kupanda miti katika zahanati hiyo iliyopo katika Kata ya Kikuyu Kaskazini jijini Dodoma.

Shekimweri alisema “niungane na Mheshimiwa Mbunge kuwapongeza kwa dhati Zahanati ya Kikuyu ikiongozwa na Mganga Mfawidhi kwa wazo la kuboresha mandhari ya zahanati yao. Ni dhamira yetu tutafute ‘model’ ya uangalizi wa mazingira katika maeneo yetu ya kutolea huduma ya afya. Mbunge amening’ata sikio kuwa atabadilisha paa siyo kwa kupaka rangi bali yeye ataleta mabati mapya”.

Aidha, alitoa rai kwa vituo vingine vya afya kuboresha mandhari yake. “Rai kwa vituo vingine vya afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuboresha mandhari. Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma upo hapa. Ninakupongeza kwa kazi nzuru unayoifanya kwa kujenga timu nzuri kwenye divisheni yako pametulia hapana mvutano, lililofanyika hapa likaakisi maeneo mengine.

Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method aliyenyoosha mkono wa kuume


Ikumbukwe kuwa Zahanati ya Kikuyu ilianza mwaka 1970 ikiwa ni moja ya zahanati kongwe katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma