WANANCHI CHAMWINO WAJITOKEZA USAFI WA MAZINGIRA

Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO

KATA ya Chamwino iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma yatekeleza zoezi la usafi wa kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kwa wananchi kijitokeza kwa wingi na kufanya usafi katika maeneo ya jumuiya.

Zoezi la usafi likiendelea


Afisa Mtendaji Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alisema kuwa zoezi la usafi wa pamoja wa kila siku ya Jumamosi ya mwisho wa mwezi lilifanyika katika mitaa minne ya kata hiyo. “Nikuhakikishie kuwa usafi wa Jumamosi ya mwisho wa mwezi umefanyika katika mitaa yote minne ya Kata ya Chamwino. Mtaa wa Nduka, Mailimbili, Sokoine na Mwaja” alisema Nkelege.

Akiongelea maeneo yaliyofanyiwa usafi wa pamoja, aliyataja kuwa ni makorongo, kusafisha mitaro na maeneo ya biashara. “Mtaa wa Mwaja na Nduka iliungana na kufanya usafi wa pamoja katika korongo. Usafi huo ulihusisha kuondoa mifuko ya plastiki, kufyeka vichaka na nyasi zilizoota ndani ya korongo. Mtaa wa Mailimbili usafi wa pamoja ulifanyika katika mtaro wa barabara ya kwenda Arusha. Usafi huo ulihusisha kutoa taka ngumu kama makopo, mifuko ya plastiki na kufyeka vichaka na vyasi zilizoota pembezoni mwa barabara na mtaro” alisema Nkelege.

Aliongeza kuwa wakazi wa Kata ya Sokoine walifanya usafi katika makazi yanayowazunguka na maeneo ya biashara.

Kata ya Chamwino iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa mstari wa mbele kuhamasisha wananchi wake kushiriki mazoezi ya usafi wa pamoja na kuwa mfano wa kuigwa katika utekelezaji wa maelekezo ya serikali.




MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma