Msalato wamshukuru Rais, Dkt. Samia ujenzi wa shule
Na. Dennis Gondwe, MSALATO WANANCHI wa Kata ya Msalato iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamemshukuru Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea shule mpya na kuwapunguzia wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata elimu. Afisa Mtendaji Kata ya Msalato, Devotha Selufara akimuelezea Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alichoifanyia Kata ya Msalato Shukrani hizo zilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Msalato, Devotha Selufara alipokuwa akiwatambulisha wataalam wa kata yake katika Shule ya Msingi Chikole kwa mgeni rasmi Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma. Selufara alisema “Shule ya Msingi Chikole ina wanafunzi 790 ilianza mwaka jana mwezi Julai. Baada ya kumaliza ujenzi ulioanza mwezi Aprili, 2023 kwa fedha ya mama Samia Suluhu Hassan aliyotupatia shilingi 318,800,000 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya msingi Chikole, ambapo tulijenga madarasa tisa, matundu 16 ya vyoo, jengo la utawala moja, tumefanikiwa kujenga madarasa ya chekechea ya mfano...
Comments
Post a Comment