Dodoma Jiji FC inafukuza Mwizi Kimya Kimya
Na. Mussa Richard, DODOMA
Timu
ya Soka ya Dodoma Jiji FC, imeendelea na maandalizi ya kujiwinda na michezo ya
Ligi kuu ya NBC Tanzania bara, kwasasa imekita kambi mkoani Arusha, na imecheza
mchezo wa kirafiki dhidi ya timu inayoshiriki Ligi Daraja la kwanza Mbuni FC,
mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha na Dodoma
Jiji FC kuchomoza na ushindi wa bao 1-0.
Akizungumza
baada ya mchezo kutamatika Kocha wa Viungo wa Dodoma Jiji FC, Fransis Mkanula
alisema “tumekuja hapa Arusha kuweka kambi ya siku tano, tumekuja hapa kupata
mechi za kirafiki kwasababu timu imetoka kwenye mapumziko, baada ya ratiba
kutoka tukaamua kuja hapa Arusha kucheza mechi za kirafiki ili kurudisha
utimamu wa miili kwa wachezaji pia ukizingatia tuna maingizo mapya kwenye timu.
Kwahiyo, tumekuja kutengeneza mazingira ya kuzoeana na wenzao na kuingia kwenye
mfumo wa timu”.
Nae,
Nahodha wa Dodoma Jiji FC, Augustin Nsata akaelezea hali ya kambi na maandalizi
ya timu kuelekea kwenye michezo ya Ligi kuu ya NBC Tanzania Bara. “Hali ya
kambi ni nzuri na hali ya hewa ya Arusha ni nzuri, tumekuja Arusha kwasababu
kuna timu nzuri na zenye ushindani ambazo zitatupa kujua hali ya timu yetu. Kwasasa,
jambo ambalo kwa mwalimu yeye anaona kama kuna madhaifu kwenye timu tukirudi
uwanja wa mazoezi tukarekebishe ili kwenye mchezo wa kirafiki unaofuata tuweze
kufanyia kazi maelekezo ya mwalimu”. alisema Nsata.
Mpaka
sasa Dodoma Jiji FC imecheza michezo miwili ya kirafiki dhidi ya Mtibwa Sugar
mchezo ulioisha kwa suluhu ya kufungana mabao 2-2, mchezo mwingine Dodoma Jiji
FC, walishuka dimbani kuwakabiri Mbuni FC ambapo Dodoma Jiji FC ilishinda kwa
bao 1-0, Dodoma Jiji FC imebakiza mchezo mmoja wa kirafiki ambao itacheza na
timu ya Gunners FC.
MWISHO
Comments
Post a Comment