Ofisi ya Kata Zuzu yaboreshwa kwaajili ya utoaji huduma bora

Na. Leah Mabalwe, ZUZU

Serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imelenga kuboresha mazingira bora ya kufanyia kazi kwa watumishi wa serikali ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi.



Hayo yalibainishwa na Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Zuzu, Shakila Mwanyemba, alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita ndani ya robo ya tatu 2024/2025 wakati wa ziara iliyofanywa na Kamati ya Fedha na Utawala katika Kata ya Zuzu.

“Serikali ya awamu ya sita ilitenga kiasi cha shilingi 15,000,000 kwaajili ya ukarabati wa Ofisi ya Kata ya Zuzu, ikiwa ni chachu ya kuboresha mazingira bora kwaajili ya watumishi ili waweze kutoa huduma nzuri kwa wananchi. Pia ofisi hii siyo tu kwaajili ya watumishi pekee, bali hata wananchi wanaweza kuja kupata huduma bora katika ofisi hii kutokana na mazingira ya ofisi kuwa bora, salama na rafiki” alisema Mwanyemba.



Nae, Awadhi Abdallah, Diwani wa Kata ya Zuzu alitoa pongezi kwa serikali kwa kuendelea kuboresha utawala bora na kuwasogezea wananchi huduma katika maeneo yao. “Serikali ya awamu ya sita imeendelea kuwasogezea huduma bora wananchi wake ikiwemo huduma za kijamii kama vile ujenzi wa shule, ujenzi wa barabara, vituo vya afya pamoja na kujenga ofisi za kata ili wananchi waweze kupata huduma za kijamii karibu na maeneo yao ya kuishi. Kwahiyo, nitoe pongezi kwa serikali pamoja na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuendelea kuratibu na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi” alisema Abdallah.

MWISHO

                       

 

Comments

Popular Posts

Osterbay Dodoma wajitokeza usafi wa mazingira

Usafi wa Mazingira Kipaumbele Kata ya Chamwino

Wananchi wa Kata ya Mtumba wanufaika na Mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri