PROF. MWAMFUPE APONGEZA UFANISI KLINIKI YA ARDHI DODOMA

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe amepongeza ufanisi wa Kliniki ya Ardhi inayoendelea jijini hapa na kusema ni mafanikio makubwa.

Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe akitoa pongezi kwa Kliniki ya Ardhi Jiji la Dodoma


Pongezi hizo alizitoa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa robo ya kwanza uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri.

Prof. Mwamfupe ambae ni Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema “kniliki hiyo ni muendelezo wa mafanikio katika sekta ya Ardhi. Jana pekee zimetolewa hati 217, zikijumuisha maombi yaliyopokelewa papo kwa hapo. Tuendelee kutoa mapendekezo ya namna ya kuboresha kliniki hii”.

Katika hatua nyingine, Prof. Mwamfupe ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Fedha na Utawala alimteua Diwani wa viti maalum, Rosemary Nitwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala.

 “Waheshimiwa madiwani, mtakumbuka Mheshimiwa Grace Milinga alikuwa mmoja wetu hapa akiwa Diwani na alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala na alijiuzuru nafasi hiyo. Naomba mridhie kuteuliwa kwa Mheshimiwa Rosemary Nitwa kuziba pengo hilo” aliomba Prof. Mwamfupe na madiwani kuridhia.

Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakifuatilia mkutano


MWISHO

Comments

Popular Posts

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala

Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota