AWAMU II YA KLINIKI YA ARDHI JIJI LA DODOMA KUTATUA MIGOGORO KATA KWA KATA
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
Wizara
ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji
la Dodoma inaendesha Kliniki ya Ardhi kwa lengo la kutatua migogoro ya Ardhi na
kuwaondolea kero wananchi.
Kauli
hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo
alipokuwa akitoa taarifa ya katibu katika Mkutano wa Baraza la Madiwani kwa
ajili ya kupokea taarifa za utendaji kazi kwa kamati za kudumu za halmashauri kwa
kipindi ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/2024 uliofanyika katika ukumbi
wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
Kayombo
alisema “baada ya Kliniki ya Ardhi ya kwanza kufanikiwa vizuri, tumeendelea na
kliniki ya pili iliyoanza Jumamosi tarehe 4 Novemba na itaendelea hadi tarehe
20 Novemba, 2023. Tumepanga watu kikata, kwa siku tunasikiliza na kuhudumia kata
nne. Baada ya tarehe 20 tutajipima tena kuona tumefanikiwa kiasi gani na kama
watu bado wanashida zoezi litakuwa endelevu. Tunaishukuru Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi, wakurugenzi wake wote, Katibu Mkuu, Mheshimiwa
Waziri wa Ardhi wametoka ofisini tumeungana nao kwenye Kliniki ya Ardhi Dodoma”.
Aidha,
aliwaomba madiwani kuwahimiza wananchi wenye changamoto za Ardhi kujitokeza kwa
wingi katika kliniki hiyo kwa kuzingatia ratiba ya kata husika. “Kwa kuwa tumezipanga
kata kwa tarehe husika kili tupate muda mzuri wa kuwahudumia wananchi, wito
wangu waheshimiwa madiwani kuwahimiza wananchi kujitokeza wakiwa na nyaraka
husika” alisema Kayombo.
Akichangia
Diwani wa Kata ya Mtumba, Edward Maboje alishauri kuwa kliniki hiyo wakati
mwingine iwe inakwenda maeneo ya pembezoni kusikiliza kero za Ardhi. “Tunaomba
hiyo kliniki iwe inatembea kwa ajili ya kuwafikia wale wasiojiweza katika
maeneo ya pembezoni. Wapo wananchi wenye migogoro ya Ardhi ila hawana uwezo wa
kufika mjini” alisema Maboje.
MWISHO
Comments
Post a Comment