Madiwani Jiji la Dodoma wapo tayari kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MADIWANI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapo tayari kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa asilimia 100.

Mwakilishi wa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Daud Mkhandi alipotoa salamu katika Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024


Kauli hiyo ilitolewa na Mwakilishi wa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Daud Mkhandi alipotoa salamu katika Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 lililofanyika katika uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma.

Mkhandi ambae ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji na Mazingira alisema “kwa niaba ya waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, tupo tayari kushiriki zoezi la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa asilimia 100. Waheshimiwa Madiwani tupo tayari kuwahamasisha wananchi kwenda kujiandikisha. Waheshimiwa Madiwani tupo tayari kuwahamasisha wananchi kupiga kura ili kupata viongozi mahili watakaosaidia maendeleo ya wananchi wetu”.

Bonanza la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 lilitanguliwa na ‘jogging’ iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma pamoja na watumishi wa umma kwa kupita katikati ya Jiji la Dodoma kuelekea Shule ya Sekondari Dodoma chini ya kaulimbiu isemayo “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi”.




MWISHO

Comments

Popular Posts

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

Umeme wa REA chachu ya viwanda vidogo vidogo Kata ya Ipala

Kata ya Ipala ipo mstari wa mbele katika Michezo