“Maandalizi Uandikishaji Uchaguzi Serikali za Mitaa yamekamilika” Dkt. Sagamiko

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko amesema kuwa maadalizi katika uandikishaji kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa yamekamilika kwa asilimia mia moja.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko akifafanua jambo


Dkt. Sagamiko alitoa kauli hiyo wakati akimkaribisha mgeni rasmi kufungua Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 katika uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma.

Msimamizi huyo alisema kuwa maandalizi katika uandikishaji kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa yamekamilika. Vifaa vyote vimefika na rasilimali fedha, Rais amewezesha kwa asilimia mia moja. “Kwa maandalizi, tupo timamu. Matamanio yetu tukamilishe zoezi la uandikishaji katika siku tatu” alisisitiza Dkt. Sagamiko.

Aidha, aliwapongeza watumishi na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushiriki ‘jogging’ na Bonanza la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Pia alipongeza maandalizi mazuri ya Bonanza hilo kubwa la kihistoria katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki machakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 lilikuwa na michezo ya riadha, mbio za magunia, kukimbiza kuku, kukimbia na glasi, kuvuta Kamba, kukimbia na yai kwenye kijiko, mpira wa miguu, mpira wa mikono, bao, drafti, karata, kunywa soda na kukuna nazi wanaume chini ya kaulimbiu isemayo “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi”.

.





MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma