Barabara za Mtaa wa Mbwanga yafunguliwa, Diwani Kerenge aitaja kuwa chachu ya maendeleo
Na. Mwandishi wetu, Dodoma Wakazi wa Mtaa wa Mbwanga katika Kata ya Mnadani wanatarajia kunufaika na usafiri rahisi, kuimarika kwa shughuli za biashara na kuongezeka kwa fursa za maendeleo kufuatia ufunguzi wa barabara za mtaa katika uboreshaji wa miundombinu kwa ajili ya maisha bora ya wananchi. Akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa barabara hiyo, iliyofanyika katika moja ya barabara hizo, Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge alisema kuwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara ni nguzo muhimu ya maendeleo kwa kuwa unarahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa, kuchochea biashara na kuongeza upatikanaji wa huduma za kijamii. “Kukamilika kwa barabara zaidi ya kilomita 14 zimefunguliwa hii ni hatua muhimu katika safari ya maendeleo ya Kata ya Manadani. Itaondoa changamoto zilizokuwa zikiwakabili wananchi, hasa wakati wa mvua, na kufungua fursa zaidi za kiuchumi kwa wakazi wa Mbwanga na maeneo jirani. Natoa shukrani kwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kutuwezesha kufani...
Comments
Post a Comment