Chigongwe watakiwa kujitokeza kupiga kura

Na. Dennis Gondwe, CHIGONGWE

WAKAZI wa Kata ya Chigongwe, Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 27 Novemba, 2024 ili waweze kuwachangua viongozi wanaowafaa.


Masima Masima (wa pili kushoto) wakati wa kuhamasisha umma 


Kauli hiyo ilitolewa na mkazi wa Kata ya Chigongwe, Masima Masima alipokuwa akiwahamasisha wananchi wa kata hiyo kujitokeza siku ya kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa alipopata nafasi ya kuhamasisha wakati timu ya uhamasishaji ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilipofika katani hapo kutoa hamasa kwa wananchi.

Masima alisema “mimi binafsi cha kwanza, kupiga kura ni jukumu langu na ni haki yangu ya msingi. Tarehe 27 Novemba, mwaka huu ni siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Tunakwenda kumchagua mwenyekiti na wajumbe wake, mimi Masima nipo tayari kushiriki uchaguzi huo”.

Kwa upande wa mkazi mwingine wa kata hiyo, Salome Nguji alisema kuwa wanachohitaji wapate kiongozi bora siyo viongozi wa mchongo ili wawasaidie. “Tunahangaika na maji, zahanati na shule. Mwenyekiti na wajumbe wa serikali ya mitaa watusaidie. Hivyo, nina wahimiza tujitokeze kwenye kupiga kura hiyo tarehe 27 Novemba, 2024” alisisitiza Nguji.

Wakati huohuo, wafanyabiashara wa Kata ya Chigongwe walisema kuwa wapo tayari kujitokeza siku ya kupiga kura na kuwachangua viongozi wanaowahitaji.

Zoezi la kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa linatarajia kufanyika tarehe 27 Novemba, 2024 chini ya kaulimbiu isemayo “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi”.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma