Ujenzi wa madarasa 3 S/M Mazengo kukamilika Julai, 2026
Na. Mwandishi wetu, KIKUYU KASKAZINI
Uongozi wa Mtaa wa Kigamboni, Kata ya Kikuyu Kaskazini
umepongeza kasi ya ujenzi madarasa matatu katika Shule ya Msingi Mazengo kwa gharama
ya shilingi 71,373,640 kwa lengo la kuboresha mazingira ya wanafunzi kujifunzia
na kuelekeza mradi huo kukamilika kwa wakati.
Pongezi hizo zilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Kigamboni, Farijala Kunga alipoongoza wajumbe wa Serikali ya Mtaa wa Kigamboni na maafisa ugani wa Kata ya Kikuyu Kaskazini kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa madarasa matatu katika Shule ya Msingi Mazengo.
Alisema kuwa wameridhika na kasi ya ujenzi wa madarasa hayo ambayo yanatarajiwa kukamilika Mwezi Julai, 2026 kabla ya shule kufunguliwa. “Ni matumaini yangu kuwa ujenzi huu utakamilika kwa muda ulipangwa ili wanafunzi watakapofungua shule waweze kuyatumia. Madarasa haya ni utekelezaji wa ahadi ya Rais, kuleta tabasamu kwa wananchi, hapa ni wanafunzi na walimu watakaotabasamu” alisema Kunga.
Mtaa wa Kigamboni unaendesha Kliniki ya siku tatu kuanzia tarehe 11-13 Juni, 2026 ya kutoa huduma kwa wananchi zikiwemo upimaji wa afya, msaada wa kisheria zikihusisha wadau wengine kama benki ya NMB, RITA, TRA na NSSF pamoja na kusikiliza na kutatua kero zao.
MWISHO
Comments
Post a Comment