Mtakwimu Mdoya mbabe Mchezo wa Drafti
Na. Shahanazi Subeti, DODOMA
Mtakwimu wa Jiji la Dodoma, William Mdoya
ameibuka mshindi katika Mchezo wa Drafti baada ya kumfunga Afisa Michezo, Peter
Ititi kwa jumla ya mabao 2-1 ambapo mchezo huo ulilazimika kwenda kwenye muda
wa ziada baada ya muda wa kawaida kufungana bao 1-1.
Baada ya ushindi huo alisema “nafurahia
ushindi kwa sababu ndio kitu nilichokuwa nakitarajia katika bonanza hili, mchezo
ulikuwa mzuri, wachezaji wote niliokutana nao walikuwa wazuri na walionesha
ushindani ndiyo maana katika mchezo wa fainali tulienda hadi muda wa ziada”
alisema Mdoya.
Nae, Mwalimu Stephen Sebastian, ambaye ni
mmoja wa washiriki wa mchezo wa Drafti amekiri kushindwa, hii ni kutokana na
ubora wa mpinzani wake. “Mpinzani wangu alikuwa ni mzuri na anaonekana ni
mzoefu katika kucheza drafti na katika mchezo ninakiri kwamba, kuna kushindwa
na kushinda na nakubali mpinzani wangu amenizidi mbinu na ujanja katika mchezo
huu” alisema Sebastian.
Kwa upande wake Mwamuzi wa Mchezo wa Drafti,
Evance Msilu, ametoa ufafanuzi wa mchezo na kuweza kumpata mshindi katika
mashindano hayo. “Mchezo ulikuwa ni wa kishindani zaidi kwasababu fainali
ilikuwa ni ya moto, kulikuwa na timu nane kwa kila idara lakini idara nyingine zilishindwa”
alisema Msilu.
Mchezo huo umechezwa leo katika Uwanja wa
Jamhuri Dodoma na ulihusisha wafanyakazi wote wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma
katika CCD Watumishi Bonanza lililoandaliwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma
kwa ajili ya kuukaribisha Mwaka 2025 likiongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Halmashauri ya Jiji la Dodoma 2025
Ushirikiano na Umoja Wetu Ndiyo Nyenzo ya Huduma Bora.
MWISHO
Comments
Post a Comment