Shilingi 698,800,161 zatekeleza mradi wa Nishati safi Sec Dr. Samia- Dodoma
Na. Dennis Gondwe, IYUMBU
SHILINGI
698,800,161 za utekelezaji wa mradi wa Nishati safi ya kupikia katika Shule ya
Sekondari Dr. Samia-Dodoma zimelenga kuhifadhi Mazingira kwa kurejesha taka,
kupunguza matumizi ya kuni na mkaa na kulinda afya za watumiaji.
Kauli
hiyo ilitolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Dr. Samia-Dodoma, Mwl. Leticia
Singo alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa nishati safi ya kupikia kwa Kiongozi
wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2026 shuleni hapo.
“Ndugu
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, lengo la mradi ni kuhifadhi Mazingira
kwa kurejesha taka zinazozalishwa shuleni pamoja na kupunguza madhara
yatokanayo na matumizi ya kuni na mkaa kwa kutumia nishati safi ya kupikia”
alisema Mwl. Singo.
Alisema
kuwa mradi huo ulitekelezwa kwa gharama ya shilingi 698,800,161 fedha kutoka
mradi wa P4R chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia chini ya Mkandarasi
SUMA JKT. Akiongelea mafanikio ya mradi huo, aliyataja kuwa ni mradi umepunguza
gharama za ununuaji wa gesi kutoka kg 800 hadi kg 400 kwa mwezi jambo
lililookoa shilingi 12,000,000 kwa mwaka. Mafanikio mengine aliyataja kuwa
mradi umesaidia kuweka mazingira katika hali ya usafi na kurahisisha utendaji
kazi.
Nae
mkazi wa Kata ya Iyumbu, Mussa Ipyana alisema kuwa maono ya rais kuhusu
matumizi ya nishati safi yanatakiwa kuungwa mkono na watanzania wote.
Kiongozi
wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026, Wazo Mwangónda alizindua mradi
huo na kuishukuru serikali kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika. Alisema kuwa mfumo
wa nishati safi ya kupikia unapunguza gharama za upishi shuleni hapo. Aidha,
aliishauri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kusimika mfumo huo katika
shule nyingine za sekondari.
Shule
ya Sekondari Dr.
Samia-Dodoma ilisajiliwa tarehe 05
Julai, 2023 sasa ina jumla ya wanafunzi 608, walimu 30 na
wafanyakazi wasio walimu 09.
MWISHO
Comments
Post a Comment