Jiji la Dodoma latenga Bil. 3.9 kuongeza miundombinu mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2027

Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KUSINI

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetenga shilingi 3,956,990,000 katika Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuongeza miundimbinu ya madarasa, viti, meza na matundu ya vyoo ikiwa ni maandalizi ya kupokea wanafunzi watakaohitimu darasa la sita na saba kwa pamoja.



Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Wella, Mwl. Allen Lugemalila wakati akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Sekondari Wella kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026, shuleni hapo.

Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, halmashauri inategemea kupokea wanafunzi watakaohitimu darasa la sita na la saba kwa pamoja mwaka 2027. Katika kufanikisha mpango huo wa serikali, kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027, halmashauri imetenga bajeti ya shilingi 3,956,990,000 kwa lengo la kuongeza miundombinu ya madarasa, vyoo, viti na meza. Pamoja na lengo hili la msingi, shule hii ilikuwa na uhitaji wa vyumba viwili vya madarasa ili kuweza kukidhi ongezeko la ufaulu kwa wanafunzi waliohitimu darasa la saba 2025” alisema Mwl. Lugemalila.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda aliipongeza serikali kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya elimu na kuwawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira mazuri.





Shule ya Sekondari Wella ilisajiliwa tarehe 06 Januari, 2008 ikiwa na jumla ya wanafunzi 915 na walimu 66 ikiendelea kuiishi kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru isemayo ‘Tanzania ni yetu sote, tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo’.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lawafukuza kazi watumishi watatu na mmoja kushushwa cheo