Timu ya Jiji la Dodoma yajinoa kuelekea SHIMISEMITA Mbeya, 2026
Na. Mwandishi Wetu, Dodoma MSAKO wa kutetea ubingwa wa mashindano ya Shirikisho la Michezo la Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) umeanza rasmi kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma baada ya watumishi wake kushiriki bonanza la michezo lililozikutanisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na Halmashauri ya Wilaya ya Gairo katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma. Bonanza hilo limekuwa sehemu ya maandalizi ya kuelekea mashindano ya SHIMISEMITA yanayotarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu jijini Mbeya, ambapo halmashauri mbalimbali nchini zitachuana kuwania ubingwa katika michezo tofauti. Akizungumza baada ya bonanza hilo, Afisa Michezo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Neema Kilongola alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na mechi hizo zimewapa nafasi ya kupima uwezo wa kikosi kabla ya kuelekea Mbeya. “Bonanza hili limetupa nafasi ya kujipima, kurekebisha mapungufu na kuongeza ushindani ndani ya timu. Mwaka jana tulikuwa mabingwa, hivyo mwaka h...

Comments
Post a Comment