Popular Posts
Ujenzi wa Darasa Sekondari Anthony Mavunde kupunguza msongamano kwa wanafunzi
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Nancy Kivuyo, HOMBOLO BWAWANI Mkuu wa Shule ya Sekondari Anthony Mavunde, Mwalimu Emmanuel Magumba amesema kuwa shule hiyo ilipokea kiasi cha shilingi 15,425,000 kwa ajili ya ujenzi wa darasa moja na ununuzi wa viti 50 na meza 50 kwa lengo la kuongeza miundombinu katika shule hiyo. Mwl. Magumba alisoma taarifa ya mradi huo mbele ya Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kusema kuwa pamoja na ujenzi unaoendelea anaiomba halmashauri iwaongezee fedha kwa ajili ya kumalizia darasa hilo. “Hatua tuliyofikia ni nzuri kwasababu umaliziaji darasa hili sio mkubwa kama unavyoanza ujenzi” alisema Mwl. Magumba. Aliongeza kuwa kukamilika kwa darasa hilo kutaleta chachu ya wanafunzi kusoma kwa bidii. “Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa ujenzi wa darasa hili ukikamilika naamini wanafunzi wetu watapata nafasi ya kusoma na wataongeza bidii katika masomo” aliongeza Mwl. Magumba. Nae, Mwanafunzi wa Kidato cha Kwanza, Emmanuel Mbega alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwajen...
Elimu Sekondari Jiji yawalaza chali Maafisa Watendaji Mchezo wa Pete
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Halima Majidi, DODOMA Katika mchezo uliovuta hisia za mashabiki wengi, Timu ya Mchezo wa Pete ya Elimu Sekondari ya Jiji la Dodoma imeibuka kidedea kwa kuishinda Timu ya Maafisa Watendaji wa Kata na Mitaa Jiji la Dodoma goli 3-2. Mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma ulidhihirisha ushindani mkali kati ya timu hizo mbili. Mchezo ulianza kwa kasi huku wachezaji wa Elimu Sekondari wakionesha umahiri wa hali ya juu katika kurusha mpira kwa haraka na ukabaji imara. Katika robo ya kwanza, timu hiyo iliongoza kwa alama 2 dhidi ya 0 za Maafisa Watendaji. Kocha wa Timu ya Elimu Sekondari, Mwl. Zainabu Abdallah, alisema amefanya yake katika kuhakikisha wanachukua ushindi japokuwa mvua imekuwa kikwazo, na aliwapongeza vijana wake kwa kujituma uwanjani na kutumia mbinu walizofanyia mazoezi, na pia alisisitiza wachezaji wawe na tabia ya kufanya mazoezi sio tu mpaka wakti wa michezo au bonanza bali iwe ni tabia endelevu. “ Ushindi huu ni matokeo ya nidhamu, maz...
Comments
Post a Comment