Mstahiki Meya Chaula ashauri Baraza kutumia mkakati wa hoja kwa hoja
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA
Mstahiki
Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula ameshauri Baraza la
Madiwani kujenga utaratibu wa kuwasilisha hoja moja na kuiazimia hadi itakapokamilika
ndio hoja nyingine ifanyiwe kazi.
Aliyazungumza hayo kwa msisitizo katika mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri jijini Dodoma.
Alisema
kuwa mkakati huo wa hoja moja ‘Focus Strategy’ ndiyo njia pekee ya kuleta
maendeleo yanayoonekana na yenye tija kwa wananchi wanaowaongoza. "Ili
tuwe na ufanisi, niwaombe kwa unyenyekevu mkubwa sana tuchague jambo moja na
kuliazimia hadi mwisho. Kwa mfano, kama baraza linaona kipaumbele ni ujenzi wa
matundu ya vyoo kwa shule zote za msingi katika jiji letu, basi nguvu, fedha,
na usimamizi wetu wote uelekezwe hapo. Tukimaliza na kujiridhisha kuwa kila
shule ina vyoo bora, ndipo tunahamia hoja nyingine ya msingi na kuendelea na
mtiririko huo" alisema Chaula.
Alimalizia
kwa kutoa rai kuwa umoja na maamuzi ya pamoja yatawasaidia kuwa kitu kimoja na
kwamba washirikiane kuhakikisha shughuli za kimaendeleo za Jiji la Dodoma zinafaniwa.
MWISHO
Comments
Post a Comment