Jiji la Dodoma lashauriwa kulinda hadhi ya Makao Makuu ya Nchi
Na. Mwandishi wetu, DAR ES SALAAM HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeshauriwa kuendelea kusimamia Mpango Kabambe wake ili kuhakikisha jiji linakuwa na mpangilio wa kisasa na kulinda hadhi ya makao makuu ya nchi. Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Jenifa Omolo (kushoto) akiongea na wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Jenifa Omolo alipotembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. Julius Nyerere jijini hapa. Alisema kuwa ukuaji wa Jiji la Dodoma unapaswa kwenda sambamba na upangaji bora wa maeneo, miundombinu na mazingira ya mji ili kuongeza mvuto zaidi kwa wakazi, wawekezaji na wageni wanaofika kwa shughuli mbalimbali za kiserikali na kiuchumi. Alisisitiza kuwa taswira ya mji ambao ni makao makuu ya nchi inapaswa kuonekana wazi kupitia mpangilio wa kisasa, unaozing...
Comments
Post a Comment