Dodoma English Medium kusomesha kwa gharama nafuu
Na. Mwandishi wetu, MRADI wa ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi Dodoma English Medium umewasaidia wazazi wenye kipato cha kati kusomesha watoto wao katika shule ya mchepuo wa kiingereza karibu na maeneo yao kwa gharama nafuu. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Myalla alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi ya Dodoma English Medium kwa Kiogozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2024. Akiongelea faida za mradi huo alizitaja kuwa ni kuwasaidia wazazi wenye kipato cha kati kupata fursa ya kusomesha watoto kwenye shule ya mchepuo wa ki i ngereza . Faida nyingine aliitaja kuwa ni wananchi kusogezewa huduma ya shule karibu ambapo watoto walikuwa wanasafiri umbali mrefu kufuata huduma ya elimu pia wanafunzi wanapata elimu bora kwa gharama nafuu ukilinganisha na shule binafsi . “ Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024, m radi umelenga kutoa elimu bora amb...
Comments
Post a Comment