DIWANI KATA YA MNADANI ASHIRIKI KIKAO CHA WAZAZI MIYUJI SEKONDARI
Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge amepata wasaa wa kuzungumza na wazazi wa wanafunzi wa shule ya sekondari Miyuji.
Katika kikao hicho Diwani Kerenge alisisitiza umuhimu wa wazazi kushirikiana na walimu katika kusimamia watoto ili kuongeza ufaulu shuleni hapo. Pia alisisitiza kuendeleza uwazi dhidi ya michango ya wazazi wanayotoa katika shule hiyo.
Alitoa wito kwa wazazi na walimu
kuhakikisha watoto wote wanapata chakula shuleni chenye virutubisho ili
kuongeza uwezo wa kusoma vizuri wakati wote wanapokuwa shuleni.
Diwani Kerenge aliwashauri wazazi
kuhakikisha watoto wote wanakaa kambi hasa madarasa ya mitihani ili wapate muda
wa kusoma vizuri.
Comments
Post a Comment