Kimaro: Wananchi Dodoma waalikwa kuupokea Mwenge wa Uhuru Juni, 1 2026
Na.
Mwandishi Wetu, DODOMA
Mwenyekiti
wa Kamati ya Chakula katika maandalizi ya Mwenge wa Uhuru 2026 Wilaya ya Dodoma,
Dickson Kimaro anawaalika wananchi kushiriki mapokezi ya mbio za Mwenge wa Uhuru na kuwakumbusha kuwa tukio hilo
linawaungansha pamoja na kujenga mshikamano wa kimaendeleo.
Mwenyekiti wa Kamati ya huduma ya Chakula Wilaya ya Dodoma
Aliyasema
hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mapokezi ya
mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma unaotarajiwa kuwasili tarehe 1 Juni,
2026 na kukimbizwa katika miradi saba ya maendeleo.
Alisema
kuwa maandalizi yanaendelea vizuri. “Maandalizi mpaka leo hii yapo vizuri na Kamati
ya Chakula imejipanga katika eneo la chakula kwa kuhakikisha wote wanaohudhuria
wanapata chai itakayotolewa katika Shule ya Sekondari, Dkt. Samia na chakula
cha mchana kitakuwepo pale katika Shule ya Sekondari Umonga. Chakula cha usiku kitapatikana
katika shule ya Msingi Kizota’’ alisema Kimaro.
Kimaro
ambae pia ni Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti wa taka ngumu Jiji la Dodoma
alisema kuwa kitengo kipo tayari
kuupokea Mwenge wa Uhuru 2026 na kutoa wito kwa wananchi wote kujitokeza
kwa wingi kuupokea na kuukimbiza Mwenge wa Uhuru katika miradi yote wilayani
Dodoma.
Mwenge
wa Uhuru 2026 utawasili katika Wilaya ya Dodoma tarehe 1 Juni, 2026 ukiongozwa
na kaulimbiu isemayo ’’Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo’’.
MWISHO
Comments
Post a Comment