Jiji latoa 25,000,000 kumalizia Bweni Mbalawala Sec
Na. Nancy Kivuyo, NALA
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma yatoa shilingi
25,000,000 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa bweni kwa Shule ya Sekondari
Nala kwa lengo la kuwaondolea wanafunzi kutembea umbali mrefu kwenda shule na kuongeza
ufaulu.
Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Afisa Elimu Sekondari
Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Fredrick Mwakisambwe alipokuwa akisoma
taarifa ya umaliziaji wa bweni, vyoo na utengenezaji wa vitanda katika Shule ya
Sekondari Nala kwa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma.
Mwl. Mwakisambwe alisema “shule hii ilianza rasmi tarehe 05 Aprili, 2005 ikiwa na wanafunzi 71. Idadi ya wanafunzi iliendelea kuongezeka mwaka
hadi mwaka na shule kukumbwa na changamoto mbalimbali, mojawapo ikiwa ni wanafunzi wengi kutembea umbali
mrefu kutoka nyumbani. Hata hivyo, changamoto hiyo ilikuwa kubwa zaidi kwa wanafunzi wa kike na
hivyo,
uongozi wa shule pamoja na bodi
waliomba kujengewa mabweni kwaajili ya wanafunzi wa kike kwa lengo la
kuwaepusha na changamoto ya kukatisha masomo lakini pia kupandisha ufaulu wao
na shule kwaujumla”.
Alisema kuwa mwishoni
mwa mwaka 2023 shule hiyo ilipokea fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la
Dodoma kiasi cha
shilingi 25,000,000 kwa awamu mbili kwaajili ya umaliziaji wa bweni moja lenye uwezo wa kulaza wanafunzi 48, vyoo matundu manne na utengenezaji
wa vitanda 25 ambavyo ni ‘double’ deka za chuma. “Fedha hiyo iliingizwa katika akaunti ya shule
tarehe 23 Agosti, 2023 kiasi
cha shilingi 15,000,000 na tarehe 20 Septemba, 2023 kiasi cha shilingi 10,000,000… Katika
kutekeleza na kusimamia mradi huu, mfumo wa ‘force account’ ulitumika kufanya malipo ya wazabuni. Pia, mkuu
wa shule aliunda kamati tatu, ambazo ni kamati ya ujenzi, kamati ya manunuzi na
kamati ya mapokezi na ukaguzi. Aidha, utengenezaji wa vitanda 25 ulifanyika na
kugharimu jumla ya shilingi 5,000,000.00 tu. Kazi hizi zote zilifanyika na
kukamilika kwa gharama ya fedha ya shilingi 21,458,500 ambapo malipo ya
wazabuni yalikuwa shilingi 18,008,500, malipo ya fundi shilingi 3,090,000 na
gharama za maji shilimgi 360,000.
Aidha, kiasi cha
shilingi 3,541,500 kilibaki kama salio baada ya kukamilika kwa kazi hizo. Kutokana na changamoto kubwa ya maji hapa shuleni,
kamati iliamua kutumia kiasi hiki tajwa kuchimba na kujenga karo kubwa lenye
ujazo wa lita elfu 25 kwaajili ya kuhifadhia maji, ununuzi wa simtank moja la
lita 5000 na kufunga gata za kuvunia maji ya mvua” alisema Mwl. Mwakisambwe.
MWISHO
Comments
Post a Comment