Jiji latoa Mil 20 kukuza mtaji Kikundi cha Winning Star

 Na. Faraja Mbise, IPAGALA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma ilikipatia mkopo usio na riba wa shilingi 20,000,000 Kikundi cha Winning Star kwa ajili ya kuongeza mtaji kwa shughuli ya ufugaji kuku wa mayai na nyama na kuongeza wigo wa ajira.



Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Patrick Sebyiga wakati akisoma taarifa ya Kikundi cha Winning Star kinachojishughulisha na ufugaji wa kuku wa mayai na nyama katika Kata ya Ipagala mbele ya kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma ilitotembelea kikundi hicho.

Sebyiga alisema “lengo kuu la kikundi hiki ni kutumia fursa ya ufugaji ili kuajiri na kutoa ajira kwa wengine hasa vijana. Aidha, kujikwamua kiuchumi kwasababu kwa kufanya hivyo, kikundi kimeondoa utegemezi na umasiki kwenye familia hupungua. Matamanio ya kikundi ni kufuga kuku 10,000 kutokana na uhitaji mkubwa wa mayai hapa Dodoma.

Akiongelea mtaji wa kikundi hicho, Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Jiji huyo alisema kuwa mtaji wa kikundi hicho ulitokana na michango ya wanakikundi pamoja na mkopo wa halmashauri. “Kikundi kilianza kwa mtaji wa shilingi 6,300,000, kila mwanachama alichangia kiasi cha shilingi 1,050,000 ambazo zilipatikana kutokana na kuweka fedha kwenye vikoba. Kikundi kilianza kwa kununua kuku 500, ambapo kwa kipindi cha miaka miwili mtaji ulikuwa hadi kufikia 31,250,000. kwa kuwa na kuku 2,500 kabla ya mkopo. Halmashauri iliwapatia mkopo wa asilimia nne kiasi cha shilingi 20,000,000 kutoka mfuko wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu tarehe 30 Machi, 2023. kiasi hicho kimesaidia kuongeza kuku 1,000 pamoja na cage za kisasa za kuku, hivyo, kufikia kuku 3,500” alisema Sebyiga.

Kuhusu mafanikio ya kikundi, aliyataja kuwa ni kuweza kujilipa posha ya asilimia 30 ya mapato ya kila mwezi kutokana na mauzo ya mayai na mbolea.Kikundi kimefanikiwa kuajiri vijana wa kiume watatu na mama mmoja. Wanakikundi wamefanikiwa kutimiza ndoto yao ya kujiajiri wenyewe na kuajiri wengine. Kikundi kimefanikiwa kutoa mafunzo ya ufugaji kwa wanaokuja kukitembelea na kuongeza mabanda kwaajili ya kuku wengine” alisema Sebyiga.

Kikundi cha wanawake cha Winning Star, kilipo Mtaa wa Ilazo Mbuyuni, Kata ya Ipagala kilianzishwa tarehe 12 Desemba, 2020 kikiwa na wanachama sita. Kikundi kinajishughulisha na ufugaji wa kuku wa Mayai na Nyama, kimesajiliwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma tarehe 8 Septemba, 2022 na kati ya mkopo wa shilingi 20,000,000 kimefanikiwa kurejesha shilingi 14,000,000 na kubakiza shilingi 6,000,000 zitakazolipwa zote kufikia mwezi Juni, 2025.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Mbunge Mavunde akabidhi Kompyuta kwa Kata 41 za Jiji la Dodoma

Bilioni 9.1 yanufaisha vikundi kwa Mwaka 2020-2023

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma