JIJI LA DODOMA LATOA VIWANJA MBADALA 1,105 KWA WANANCHI

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetoa viwanja mbadala 1,105 kwa wananchi katika kutekeleza mkakati wake wa kumaliza migogoro ya Ardhi jijini hapa.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, John Kayombo akongea na waandishi wa habari

Mamia ya wananchi wakiwa katika mahema kupata huduma katika Kliniki ya Adhi Jiji la Dodoma

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa Kliniki ya Ardhi iliyo katika siku yake ya pili ya kutatua migogoro ya Ardhi jijini hapa.

Kayombo alisema kuwa wakati anafika Dodoma kulikuwa na wananchi takribani 4,000 wanaodai viwanja mbadala. “Yaani kiwanja kimoja kimegawiwa kwa mwananchi zaidi ya mmoja. Lakini mpaka sasa tumeshatoa viwanja 1,105 kufidia wale wananchi. Mpaka sasa tunadaiwa viwanja 2,895. Matarajio mpaka kufikia mwezi Desemba mwaka huu tutakiwa tumekamilisha kutoa viwanja hivyo 2,895. Kwa sababu kuna zoezi kubwa linaendelea la kupima eneo la Mahomanyika viwanja vitapatikana 7,000 na tutaoa viwanja 2,895 na kuwapatia wananchi viwanja vyao” alisema Kayombo. 

Kliniki ya Ardhi imewaweka pamoja wataalam wote wa sekta ya Ardhi ili kupokea, kusikiliza na kutatua migogoro ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma