HATI 240 ZATOLEWA SIKU YA KWANZA YA KLINIKI YA ARDHI JIJINI DODOMA
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
SIKU
ya kwanza ya utekelezaji wa Kliniki ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la
Dodoma yapokea wananchi 1,014 ikitoa Hati miliki 240 baada ya kusikiliza wananchi
514.
![]() |
Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, John Kayombo akiongea na waandishi wa habari kuhusu siku tano za Kliniki ya Ardhi katika Jiji la Dodoma |
Kauli
hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo
alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu Kliniki ya Ardhi iliyoanza
siku ya pili katika jiji hilo kutatua migogoro ya Ardhi.
Kayombo
alisema kuwa siku ya jana walipokea wananchi 1,014. “Wananchi tuliofanikiwa
kuwasikiliza jana ni 514. Katika wananchi 514 tumefanikiwa kutoa Hati 240.
Tulifanikiwa kusikiliza watu wenye migogoro 209. Wale waliobaki jana
tumeendelea nao leo asubuhi. Leo watu ni wengi kuliko jana na wameshapewa namba
na huduma zinaendelea vizuri” alisema Kayombo.
Akiongelea
matarajio ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa ni kutatua migogoro ya
Ardhi kwa kiasi kikubwa. “Lengo letu ni kuhakikisha wananchi wa Dodoma hawalii
kwa sababu ya Ardhi. Jambo hili ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais. Mheshimiwa
Rais hataki kuona wananchi wa Dodoma wanatoa machozi kwenye Ardhi ndio maana
tupo hapa kuwashughulikia wananchi wa Dodoma” alisema Kayombo.
Kwa
upande wake mwananchi wa Dodoma mjini, Mwajuma Seja alimshukuru Mungu kwa
kupata hati yake. “Mheshimiwa Mkuu wa wilaya na mkurugenzi wa jiji pia
nawashukuru sana kupata hati yangu. Sipo peke yangu wapo wenzengu 24, mimi peke
yangu ndio nimebahatika kupata Hati wenzangu wote hawajapata hata ‘control
number’ alisema Seja kwa masikitiko.
Kliniki
ya Ardhi imewaweka pamoja wataalam wote wa sekta ya Ardhi ili kupokea,
kusikiliza na kutatua migogoro ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
MWISHO
Comments
Post a Comment