WASIMAMIZI KLINIKI YA ARDHI WATAKIWA KUJALI MAKUNDI MAALUM
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
WASIMAMIZI
wa Kliniki ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kutoa kipaumbele
kwa makundi maalum yanapokwenda kupata huduma katika kliniki hiyo.
![]() |
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri akiongea na waandishi wa habari |
Rai
hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabr Shekimweri alipokuwa akiongea
na waandishi wa habari alipotembelea Kliniki ya Ardhi inayoendelea katika siku
yake ya pili jijini hapa ya kutatua migogoro ya Ardhi.
Shekimweri
alisema “niwaombe sana, mkusanyiko huu una watu mchanganyiko wapo wa umri wa
kati, watu wazima, wazee, wenye changamoto za malazi, wajawazito na wenye
ulemavu. Pamoja na utaratibu uliopangwa tuheshimu mahitaji ya haya makundi
maalum” alisema Shekimweri.
Aidha,
aliwataka wananchi wanaokwenda kupata huduma katika kliniki hiyo kwenda na
nyaraka kamili ili kuwasaidia wataalam katika kutatua kero za ardhi. “Wakati wa
kuwasilisha changamoto na kero tujitahidi kuja tukiwa tumekamilisha nyaraka za
kuunga mkono hoja tunayoijenga. USipokuwa na nyaraka husika utakuwa umepoteza
muda wako, njoo ukiwa umejipanga na nyaraka zako zote ili zitusaidie
kukuhudumia” alisema Shekimweri.
Vilevile,
aliwataka wataalam kuwahudumua wananchi wa heshima na utu. “Wataalam tuendelee
kuwasikiliza wananchi hawa kwa heshima, tutangulize utu na tuwe na kauli nzuri
kwa wananchi. Moja ya changamoto kubwa ni kauli zisizofaa kwa wananchi. Ni
lazima tutangulize heshima kwenye utendaji kazi wetu” alisisitiza Shekimweri.
Kliniki
ya Ardhi imewaweka pamoja wataalam wote wa sekta ya Ardhi ili kupokea,
kusikiliza na kutatua migogoro ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
MWISHO
Comments
Post a Comment