Barabara ya Judiciary kupunguza msongamano katikati ya Jiji la Dodoma

Na. Dennis Gondwe, TAMBUKARELI

UJENZI wa barabara ya ‘Judiciary’ yenye urefu wa kilometa mbili unalenga kupunguza msongamano wa magari katikati ya Jiji la Dodoma na kuharakisha huduma kwa wananchi.



Kauli hiyo ilitolewa na Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Dodoma, Mhandisi Emmanuel Mfinanga wakati akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa barabara ya Judiciary yenye urefu wa kilometa mbili kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa.

Mhandisi Mfinanga alisema ”ndugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2024, lengo la mradi huu ni kupunguza msongamano wa magari katikati ya Jiji la Dodoma, kurahisisha huduma kwa wananchi katika ofisi zilizopo katika eneo hili ambapo miongoni mwa ofisi hizo ni:- Ofisi ya Bima (NHIF), Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Wakala wa Ununuzi Tanzania (PPRA), Ofisi za Maadili ya Viongozi wa Umma na Ofisi za Mahakama Kuu ya Tanzania”. 



Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Godfrey Mnzava baada ya kuweka jiwe msingi mradi wa barabara ya Judiciary KM 02


Alisema kuwa eneo la NCC Link lina barabara zenye jumla ya kilomita 9.8, barabara ya ’Judiciary’ ni miongoni mwa barabara hizo. Kutokana na umuhimu wa barabara katika eneo hili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ilitenga fedha kiasi cha shilingi 2,409,187,951.00 kwa ajili ya ujenzi wa Kilomita mbili za lami ngumu, aliongeza.

Akiongelea hali ya utekelezaji wa mradi huo, alisema kuwa ulianza kutekelezwa tarehe 04 Julai, 2023 na ulitarajiwa kukamilika tarehe 13 Juni, 2024. Kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo hali ya mvua, muda wa utekelezaji uliongezwa hadi tarehe 07 Agosti, 2024. ”Mradi huu una gharama ya shilingi 2,409,187,951.00 ambapo hadi sasa kiasi cha shilingi 1,330,768,612.00 sawa na asilimia 55.24 kimeshalipwa” alisema Mhandisi Mfinanga.

Kwa upande wake mkazi wa Tambukareli, Diana Misana alisema kuwa ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami utaongeza ufanisi kwa watumishi na watu wanaotumia barabara hiyo kutokana na kuwa na taasisi nyingi jambo linalosababisha msongamano.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Osterbay Dodoma wajitokeza usafi wa mazingira

Usafi wa Mazingira Kipaumbele Kata ya Chamwino

Wananchi wa Kata ya Mtumba wanufaika na Mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri