Kituo cha Afya Ilazo mkombozi kwa wananchi
Na.
Mwandishi wetu
MRADI
wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo utakapokamilika utahudumia wananchi 99,743 wa
Kata ya Nzuguni na maeneo ya jirani ikiwa ni mkakati wa serikali ya awamu ya
sita wa kusogeza huduma za afya karibu na wananchi.
Kauli
hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri
ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akisoma taarifa mradi wa ujenzi
wa Kituo cha Afya Ilazo kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka
2024.
Dkt. Method alisema kuwa lengo
la mradi huo ni kuboresha huduma za mama na mtoto na huduma za upasuaji
ukitarajiwa kuhudumia zaidi ya wananchi 99,743 wa Kata ya Nzuguni, Ipagala na
maeneo menginge watapata huduma bora za afya mradi huo utakapokamilika.
Akiongelea
mafanikio ya mradi huo, aliyataja kuwa ni kuwezesha kutoa huduma za upasuaji, kliniki ya mama na mtoto,
huduma za kujifungua, wodi ya watoto wachanga, huduma za kuhifadhi
miili. Mafanikio mengine ni “wodi hizi pia zimeunganishwa na mifumo ya hewa
ya Oksijeni ambayo iko katika wodi ya wazazi, watoto na jengo la
upasuaji. Mifumo hii itasaidia wagonjwa wote wenye changamoto ya upumuaji
kupata huduma hapa kituoni. Aidha,
huduma za lishe zitatolewa ikiwemo elimu juu ya masuala ya lishe, upimaji wa
hali za lishe na ushauri” alisema Dkt. Method.
Kuhusu
gharama za mradi huo, alizitaja kuwa ni shilingi 3,094,983,663.32. Kati ya
fedha hizo shilingi 2,870,483,663.32 ni gharama za ujenzi na shilingi 224,500,000.00 ni kwa
ajili ya Mshauri Mwelekezi na hadi hatua hii iliyofikia kiasi cha shilingi 2,583,435,296.98
kimetumika, aliongeza.
Mradi
wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo ulianza kutekelezwa tarehe 04 Julai, 2023 na Mkandarasi Kampuni ya Salem Construction
Ltd ya S.L.P 38160 Dar es Salaam na Mshauri Mwelekezi ni Inter Consut Ltd wa
S.L.P 423 Dar es Salaam chini ya ufadhili wa KOICA kupitia shirika la
kuhudumia watoto UNICEF.
Mradi huu unatekelezwa kwa muda wa miezi (13) na unatarajiwa kukamilika tarehe
31
Desemba, 2024.
MWISHO
Comments
Post a Comment