Hazina Volleyball yaiduwaza Dodoma Jiji Seti 2-0 Mwenge Super Cup
Na. Dennis Gondwe, DODOMA
TIMU ya Wanaume ya Mpira wa Mikono ya Hazina (Hazina
Volleyball Club) imeibuka na ushindi wa Seti 2-0 dhidi ya Timu ya Dodoma Jiji mchezo
uliochezwa katika viwanja vya Chinangali Park mapema leo.
Akiongelea mchezo huo, Nahodha wa Timu ya Hazina Volleyball Club, George Kalunde alisema timu yake ilijiandaa vizuri kuelekea mchezo huo ndio sababu ya kupata ushindi wa Seti 2-0.
Aidha, aliipongeza Wilaya ya Dodoma kwa kuandaa
mashindano ya Mwenge Super Cup Mwaka 2026 na kutaja maandalizi hayo kuwa ni
ubunifu mkubwa. “Nitumie nafasi hii kuwahamasisha vijana wenzangu kujitokeza
kwa wingi kushiriki katika mapokezi na mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026
katika Wilaya ya Dodoma, karibuni sana.
Nae Nahodha wa Timu ya Mpira wa Mikono ya Dodoma Jiji,
Muhidin Mwenda alisema kuwa mchezo ulikuwa mzuri pamoja na kufugwa. “Tunapenda
kumshukuru Mungu tumemaliza mechi salama, pamoja na kuwa tumepoteza mechi kwa
seti 2-0, siyo matokeo mazuri kwetu. Mashindano haya yamekuwa chachu kwa ajili
ya kuimarisha mwili lakini yamekuwa hamasa kwa ajili ya maandalizi ya kuupokea
Mwenge wa Uhuru siku chache zijazo. Kaulimbiu isemayo ‘Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa
Pamoja Kuleta Maendeleo’ imetutia
hamasa zaidi na tunajiona ni sehemu ya kuhamasisha amani na maendeleo” alisema
Mwenda.
Comments
Post a Comment